Skip to main content

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA NJIA YA VIDEO

 Taasisi ya RafikiElimu Education Consultancy, kupitia Mradi wa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa njia ya videon( VIDEO - MAFUNZO PROJECT) inakutangazia wewe kijana wa ki Tanzania,  nafasi ya kujiunga na mafunzo ya Ujasiriamali kwa njia ya video. 


Masomo yatakayo fundishwa ni pamoja na 👇


1. Jinsi ya kutengeneza pipi za kihindi ( Pipi za Kihindi) ni pipi zinazo tengenezwa Nyumbani kwa kutumia sukari ya kawaida ama sukari guru. Pipi hizi ni pipi zinazo pendwa Sana na watoto wa shule za msingi na sekondari. Kijana akijua jinsi ya kutengeneza pipi hizi, anakuwa amepata ujuzi utakao muwezesha kujitengenezea kipato chake halali kupitia kutengeneza pipi hizo za kihindi na kwenda kuziuza mashuleni 



2. Jinsi ya kutengeneza mashine za kutotolea vifaranga wa kuku ( Incubators) 


3. Jinsi ya kutengeneza chaki. 


4. Jinsi ya kutengeneza sabuni za aina mbalimbali. 


5. Jinsi ya kutengeneza ice cream, na juice za aina mbalimbali. 


6. Pamoja na masomo mengine mengi. 


Mafunzo haya yanatolewa kwa njia ya video, hivyo unaweza kuyapata mahali popote pale ulipo ndani na nje ya Tanzania. 


Mafunzo yataanza Kutolewa rasmi siku ya Jumatatu ya tarehe 4 AGOSTI 2025.


FOMU ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO HAYA ZINAPATIKANA OFISINI KWETU CHANIKA MWISHO ( NZASA KWA MWARABU) 



Kwa wewe ulie mbali na CHANIKA au ulie nje ya Dar Es Salaam, tuandikie barua ya maombi ya fomu ya kujiunga na mafunzo haya kupitia barua Pepe yetu ambayo ni : rafikielimutanzania@gmail.com.


Au kupitia WHATSAPP number:


0745 433 595.


Mwisho wa kupokea maombi ya fomu za kujiunga na mafunzo haya ni siku ya Juamatatu ya tarehe 01 AGOSTI 2025 saa tisa kamili alasiri. 


Kwa taarifa zaidi kuhusu mradi huu pamoja na kazi zetu nyingine, tutembelee kila siku hapa hapa kwenye blogu yetu. 


Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa...

SOMO LA KWANZA : UTENGENEZAJI WA SABUNI ZA AINA ZOTE.

 MASOMO  YATAKAYO  FUNDISHWA  HAPA  NI : 1 1. Utengenezaji  Wa Sabuni  isiyo na garama. 22. Utengenezaji  Wa Sabuni ya urembo. 33. Utengenezaji  Wa  Sabuni ya asali na cream. 4 4.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya manukato. 5 5.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ngumu. 66.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya unga 77. Utengenezaji   Wa Sabuni ya kugandisha. 8 8. Utengenezaji    Wa  Sabuni za dawa. 99. Utengenezaji  Wa  Sabuni za rangi. 110.  Utengenezaji  Wa Cream ya kunyolea. 111. Utengenezaji  Wa  Sabuni iliyotengenezwa na mafuta mengine.  VIFAA     VYA     UTENGENEZAJI   SABUNI. *Sufuria. *Bakuli kubwa la mfinyanzi au plastiki. *Mafuta *Maji. *Sodium hydroxide{NaOH} *Ubao mdogo/mwiko.  *Chombo chenye ukubwa cha plastiki. *Kifyatulio. *Ki...

SOMO LA TISA : USINDIKAJI WA MAZAO YA NAFAKA

Mahindi  yaliyo  toka  kuvunwa. 1 .   USINDIKAJI  WA   ZAO  LA  MAHINDI : Ili kuongeza matumizi ya mazao hayo na kudumisha ubora wake ni muhimu teknolojia za kusindika nafaka zitumike. Usindikaji pia huongeza thamani ya zao.                             KUSINDIKA MAHINDI Punje za mahindi hutumika kupika makande na husindikwa kupata unga unaotumika katika matumizi mbalimbali. Vile vile bidhaa nyingine zinazotokana na mahindi ni mafuta na wanga. KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA Kuna aina mbili za unga wa mahindi, unga wa mahindi yasiyokobolewa(Dona) na unga wa mahindi yaliyokobolewa (Sembe)  KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA WA DONA Vifaa • Mashine ya kukoboa • Mashine ya kusaga • Ungo • Debe • Mifuko • Chekeche ya nafaka Jinsi ya kusindika • Pepeta na pembua mahindi ili kuondoa vumbi na takataka nyingine kwa kutumia chekeche, ungo a...