Skip to main content

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

RafikiElimu   Foundation     wanatangaza  nafasi za  mafunzo  ya  ujasiriamali .  Mafunzo  yatakayo  tolewa  ni  pamoja  na  :
1.   Kutengeneza  sabuni
2.  Kutengeneza    chaki
3.Kutengeneza  mishumaa.
4.Kutengeneza   viatu  vya  ngozi.
5. Kutengeneza  mkaa  kwa  makaratasi.
6. Kutengeneza  batiki.
7. Uokaji  mikate
8. Usindikaji  wa   vyakula  na  vinywaji  pamoja  na
9.  Uongozi  wa   biashara.

WALENGWA   WAKUU  WA  MAFUNZOSIFA  ZA   WASHIRIKI
Ili  uweze  kupata   nafasi  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  unatakiwa  uwe  na  sifa  zifuatazo:
1.  Uwe  raia  wa  Tanzania.
2. Uwe  na  umri  wa  kuanzia  miaka  16  na kuendelea
3. Uwe  unajua  kusoma  na  kuandika .

ADA  YA  KUSHIRIKI  KATIKA  MAFUNZO

Ada  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  ni  shilingi   Elfu  Ishirini  na  Tano  Tu (  Tshs.  25,000/=)

MALIPO  YA  ADA
Malipo  ya  ada  ya  mafunzo  yafanyike  kupitia   CRDB  BANK,  Account  number 0152395997900 ,   Jina  la  Akaunti  ni    RAFIKI  ELIMU  FOUNDATION.


             Malipo  yafanyike  kabla  ya  tarehe   28  Agosti  2012

            TAREHE  YA      KUANZA  KWA  MAFUNZO
 Mafunzo  yataanza  rasmi  siku  ya  tarehe  01  Septemba  na  yatafanyika  katika  vituo  vya   Dar  Es  salaa,  Arusha, Moshi, Mwanza, Tanga, Morogoro,Mbeya   na  Dodoma.

Kujiandikisha   katika  mafunzo  haya,  tuma  barua  yako  ya  maombi  , ikiambatana  na  nakala  ya  cheti  chako  cha  kuzaliwa  ama   nakala  ya  kadi ya  mpiga  kura, pamoja  na  nakala  ya  risiti  ya  malipo  ya  ada  ya  mafunzo    kwenda  kwa  :
Mkurugenzi  Mtendaji,
RafikiElimu   Foundation,
S.L.P  35967,
Dar  Es  salaam.


Mwisho  wa    kupokea    maombi  ni  tarehe   28  Agosti  2012.
                                    

Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa...

SOMO LA KWANZA : UTENGENEZAJI WA SABUNI ZA AINA ZOTE.

 MASOMO  YATAKAYO  FUNDISHWA  HAPA  NI : 1 1. Utengenezaji  Wa Sabuni  isiyo na garama. 22. Utengenezaji  Wa Sabuni ya urembo. 33. Utengenezaji  Wa  Sabuni ya asali na cream. 4 4.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya manukato. 5 5.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ngumu. 66.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya unga 77. Utengenezaji   Wa Sabuni ya kugandisha. 8 8. Utengenezaji    Wa  Sabuni za dawa. 99. Utengenezaji  Wa  Sabuni za rangi. 110.  Utengenezaji  Wa Cream ya kunyolea. 111. Utengenezaji  Wa  Sabuni iliyotengenezwa na mafuta mengine.  VIFAA     VYA     UTENGENEZAJI   SABUNI. *Sufuria. *Bakuli kubwa la mfinyanzi au plastiki. *Mafuta *Maji. *Sodium hydroxide{NaOH} *Ubao mdogo/mwiko.  *Chombo chenye ukubwa cha plastiki. *Kifyatulio. *Ki...

SOMO LA TISA : USINDIKAJI WA MAZAO YA NAFAKA

Mahindi  yaliyo  toka  kuvunwa. 1 .   USINDIKAJI  WA   ZAO  LA  MAHINDI : Ili kuongeza matumizi ya mazao hayo na kudumisha ubora wake ni muhimu teknolojia za kusindika nafaka zitumike. Usindikaji pia huongeza thamani ya zao.                             KUSINDIKA MAHINDI Punje za mahindi hutumika kupika makande na husindikwa kupata unga unaotumika katika matumizi mbalimbali. Vile vile bidhaa nyingine zinazotokana na mahindi ni mafuta na wanga. KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA Kuna aina mbili za unga wa mahindi, unga wa mahindi yasiyokobolewa(Dona) na unga wa mahindi yaliyokobolewa (Sembe)  KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA WA DONA Vifaa • Mashine ya kukoboa • Mashine ya kusaga • Ungo • Debe • Mifuko • Chekeche ya nafaka Jinsi ya kusindika • Pepeta na pembua mahindi ili kuondoa vumbi na takataka nyingine kwa kutumia chekeche, ungo a...