Skip to main content

Posts

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA NJIA YA VIDEO

 Taasisi ya RafikiElimu Education Consultancy, kupitia Mradi wa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa njia ya videon( VIDEO - MAFUNZO PROJECT) inakutangazia wewe kijana wa ki Tanzania,  nafasi ya kujiunga na mafunzo ya Ujasiriamali kwa njia ya video.  Masomo yatakayo fundishwa ni pamoja na 👇 1. Jinsi ya kutengeneza pipi za kihindi ( Pipi za Kihindi) ni pipi zinazo tengenezwa Nyumbani kwa kutumia sukari ya kawaida ama sukari guru. Pipi hizi ni pipi zinazo pendwa Sana na watoto wa shule za msingi na sekondari. Kijana akijua jinsi ya kutengeneza pipi hizi, anakuwa amepata ujuzi utakao muwezesha kujitengenezea kipato chake halali kupitia kutengeneza pipi hizo za kihindi na kwenda kuziuza mashuleni  2. Jinsi ya kutengeneza mashine za kutotolea vifaranga wa kuku ( Incubators)  3. Jinsi ya kutengeneza chaki.  4. Jinsi ya kutengeneza sabuni za aina mbalimbali.  5. Jinsi ya kutengeneza ice cream, na juice za aina mbalimbali.  6. Pamoja na masomo mengine mengi....
Recent posts

Vijana kutoka Dar Es Salaam, Mwanza, Mbeya, Kagera : Vinara kwenye mafunzo ya utengenezaji wa pipi za kihindi.

Mikoa ya Dar Es Salaam, Mwanza, Mbeya na Kagera  imeongoza kwa kutoa  idadi kubwa ya vijana wanao shiriki katika mafunzo ya UTENGENEZAJI WA PIPI ZA KIHINDI.  Mafunzo ya kutengeneza Pipi za Kihindi ni mafunzo yanatolowea na Taasisi ya Facility Elimu Education Consultancy, yenye makao yake makuu, Chanika, wilaya ya Ilala, mkoani Dar Es Salaam.  Katika mafunzo hayo yanatolewa kwa njia ya masafa marefu ( Distance Learning Program), idadi kubwa ya washiriki wa mafunzo hayo wanatoka katika mkoa wa Dar Es Salaam, huku ikifuatiwa na mikoa ya Mwanza, Mbeya na Kagera.  Pipi za Kihindi ni pipi zinazo pendwa sana na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.  Vijana wanao shiriki kwenye mafunzo haya, utumia ujuzi huo, kutengeneza pipi hizo majumbani mwao na kisha kwenda kuziuza kwenye shule za msingi na / au sekondari.  Mafunzo haya yame anzishwa maalumu kwa ajili ya kuwasaidia vijana walio feli kids to cha nne kwa kupata Division 4 na Zero, kupata ujuzi utakao wa...

NAFASI ZA KAZI ( FOOD PRODUCTION)

NAFASI     ZA KAZI    ( FOOD PRODUCTION )   RafikiElimu   Education Consultancy ni Taasisi inayo jihusisha na usimamizi wa maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi wanao soma katika shule za msingi na sekondari nchini Tanzania, pamoja   na mafunzo ya ujasiriamali. Taasisi   Kwa kushirikiana   na shule mbalimbali za msingi na sekondari katika mikoa ya Dar Es Salaam na Mtwara     inaratibu   mradi wa “ MAFUNZO YA UTENGENEZAJI   WA PIPI ZA VIJITI” almaarufu kama “ PIPI ZA KIHINDI”, kwa vijana waliomaliza kidato cha nne.    Lengo   la mafunzo haya ni kuwajengea    vijana hao , uwezo wa kujiajiri wenyewe   kwa kutengeneza   na kuuza pipi hizo kwenye shule za msingi na sekondari ambazo zinashirikiana na taasisi   katika mradi huu.    Kupitia mradi huu, taasisi inatangaza   nafasi za kazi   ya   kufundisha namna ya kuandaa na kutayarisha pipi za vijiti ( Pipi za kihi...

NAFASI ZA KAZI MTAFITI MSAIDIZI : NAFASI KUMI NA MBILI ( ATHARI ZA MIMBA ZA UTOTONI)

  NAFASI ZA KAZI MTAFITI MSAIDIZI : NAFASI KUMI NA MBILI ( ATHARI  ZA MIMBA  ZA UTOTONI, ENEO LA MZINGATIO, LINDI & MTWARA) RafikiElimu Education Consultancy ni Taasisi binafsi inayo jihusisha na usimamizi wa maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi wanao soma  QT pamoja na wale wanao jiandaa kurudia mitihani ya sekondari ( Re-seaters).  Taasisi ina andaa kitabu pamoja na documentary maalumu  kuhusu  ATHARI ZA MIMBA ZA UTOTONI katika wilaya mbalimbali zilizopo katika mikoa ya Lindi na Mtwara.   Kupitia project hii, Taasisi inatangaza nafasi kumi na mbili za kazi ya “ Mtafiti Msaidizi” atakae msaidia mwandishi mkuu wa kitabu hiki kupata taarifa muhimu zitakazo muwezesha kukamilisha zoezi la kuandika kitabu hiki.   MAJUKUMU YA KAZI HII : ni pamoja na kuwatafuta  wahanga  wakuu wa tatizo la mimba za utotoni yani wasichana waliopata mimba utotoni na kuharibiwa ndoto zao za kuendelea na masomo yao kwa ajili ya kufanya mah...

NAFASI ZA KAZI ( WASAIDIZI WA KAZI ZA OFISINI/ OFFICE MESSENGERS/ MESENJA WA OFISINI)

  NAFASI  ZA  KAZI ( WASAIDIZI WA KAZI ZA OFISINI/ OFFICE MESSENGERS/MESENJA WA OFISINI) RafikiElimu Education Consultancy ni   Taasisi inayo jihusisha na usimamizi wa maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi wanao soma QT ( Qualifying Test) pamoja na wale wanao jiandaa kurudia mitihani yao ya sekondari ( Re-seaters). Taasisi inaratibu na kusimamia program maalumu ya kuwasaidia   wahitimu walio feli kidato cha nne, kupata nafasi za kazi ya UMESENJA WA   OFISINI kwenye ofisi mbalimbali ili waweze kupata kipato   kitakacho wasaidia kujiendeleza kitaaluma   kupitia taasisi yetu.   Majukumu ya kazi hii ni pamoja na : kufanya usafi wa ofisi , kupika chakula cha wafanyakazi,kufua nguo za wafanyakazi, kupokea wageni wa ofisi, kutumwa kazi mbalimbali za ofisi ndani na nje ya ofisi, nakadhalika.      SIFA ZA MWOMBAJI 1. Awe wa jinsia   yoyote ( yani wa kike au wa kiume) 2.   Awe muhitimu alie feli kidato cha nn...

RC Chalamila: Dar es Salaam kufuta shule zote za sekondari za kutwa ili kudhibiti nidhamu ya wanafunzi

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema wapo kwenye mchakato wa kufuta shule zote za sekondari za kutwa kwa ajili ya kudhibiti nidhamu kwa wanafunzi wote wa sekondari. Chalamila ameyasema hayo katika uwanja wa shule ya Sekondari ya Azania kwenye hafla ya kukabidhi magari kwa maafisa elimu wa sekondari kutoka wilaya nane, ambapo amesema, Mkoa wa Dar es Saalam una shule za sekondari 182 na za binafsi zipo nyingi zaidi ya 200. --- ILI kudhibiti nidhamu kwa wanafunzi wa shule za Sekondari, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema wapo kwenye mchakato wa kufuta shule zote za Sekondari za kutwa. Chalamila ameyasema hayo leo Agosti 14, 2023 katika uwanja wa shule ya Sekondari ya Azania kwenye hafla ya kukabidhi magari kwa maafisa elimu wa sekondari kutoka wilaya nane. Amesema, Mkoa wa Dar es Saalam una shule za sekondari 182 na za binafsi zipo nyingi zaidi ya 200. “Katika Mkoa tunapokea sh billion 1.3 fedha zinazohudumia wanafunzi kama ada na posho ya madar...

Ijue RAFIKIELIMU EDUCATION CONSULTANCY

RafikiElimu EDUCATION Consultancy ni Taasisi binafsi inayo jihusisha na USIMAMIZI wa MAENDELEO ya KITAALUMA kwa wanafunzi wanao soma katika shule za sekondari Tanzania. Taasisi kwa makubaliano binafsi kati ya taasisi na mzazi/mlezi, inafanya kazi ya kufuatilia na kusimamia maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi wanao soma katika shule za kutwa ( Day Scholars ) pamoja na wale wanao soma katika shule za bweni ( Boarding Scholars ) Taasisi ina toa huduma hii kwa wanafunzi wa sekondari waliopo ndani ya mkoa wa Dar Es Salaam, pamoja na wale waliopo nje ya mkoa wa Dar Es Salaam. Vile vile, RafikiElimu EDUCATION Consultancy ina wasimamia pia wanafunzi wanao jiandaa na mitihani ya kidato cha nne, au sita kama watahiniwa binafsi ( Private Candindates ) , wanafunzi wanao jiandaa kurudia mitihani yao ya kidato cha nne au sita ( Reseaters), pamoja na wanafunzi wanao soma masomo ya...