Skip to main content

Tawla: Wanaume mnaopigwa na wake zenu jitokezeni


Ni nadra kusikia mwanamume akilalamika kuwa amepigwa na mke au mwenza wake. Suala hilo ni adimu zaidi katika nchi za Afrika hasa zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara ambazo zimefunikwa na blanketi la mfumo dume.

Kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni woga, aibu na kasumba ya mfumo dume, wanaume wanaonyanyaswa wamekuwa wakificha aibu hiyo na kuendelea kubaki katika unyanyasaji huo.

Kutokana na ongezeko la matukio ya wanaume kunyanyaswa na wake au wenza, Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania, (Tawla) kimetoa wito kwa wanaume kujitokeza ili kupata msaada wa kisheria pindi wanaponyanyaswa.

Mwenyekiti wa asasi zisizo za kiserikali za katiba na jinsia, (Zec) zinazoratibiwa na Tawla, Victoria Mandari anasema matukio hayo ni mengi lakini wanaume wamekuwa wakiyafanya kuwa siri pengine kwa kuona aibu.

“Wanaume watafute chama kitakachowasaidia kutetea haki zao na kutengeneza hata sheria ambazo zitawasaidia kupata haki zao,” anasema. Anasema sheria zinasema kuwa asiwepo mwanandoa anayemnyanyasa mwenzake kijinsia, hivyo basi hata wanaume nao hawatakiwi kunyanyaswa.

“Tatizo ni kuwa wanaume hawajitokezi wanaponyanyaswa, waseme ili wasaidiwe,” anasema.

Matukio ya wanaume kunyanyaswa na wake zao yameendelea kutokea huku wanaume wakidai kuwa unyanyasaji huo unachochewa na wingi wa vyama, asasi, na mashirika yanayotetea haki za wanawake pekee.

Mwaka jana, Naibu Kamishna wa Polisi, Adolphina Chialo alisema wanaume wengi sasa wanakwenda kushtaki katika madawati ya kijinsia ya polisi pale wanaponyanyaswa.

Inaelezwa kuwa hata wanawake wanaowanyima unyumba waume zao bila sababu maalumu nao wanafanya unyanyasaji wa kijinsia.

Kamishna Chialo anasema wapo wanaume wanaofika vituo vya polisi wakiwa na majeraha baada ya kupigwa na wake zao.

Katiba Inayopendekezwa;

Pamoja na unyanyasaji kwa wanaume, wanasheria hao walizungumzia Katiba Inayopendekezwa na kusema kuwa licha ya kupingwa na taasisi nyingi za kijinsia na kisheria nchini, kwa upande wao imezingatia masuala ya jinsia ambayo awali, hayakutambuliwa katika Katiba ya sasa.

Mandari anasema maoni yaliyotolewa na chama hicho katika Katiba Mpya yalifanyiwa kazi.

“Tumeona mambo mengi ambayo tuliyasema wakati wa kukusanya maoni kwa mfano, Katiba Inayopendekezwa sasa inatambua kabisa masuala ya ndoa, umri sahihi wa ndoa na umiliki wa mali,” anasema.

Anasema Katiba ya mwaka 1977 iliruhusu ndoa kwa msichana wa miaka 14 suala analosema liliwanyima mabinti haki ya kusoma na kuchochea unyanyasaji wa kijinsia.

“Ile sheria haikuwa nzuri kabisa, hebu fikiria mtoto mdogo anaingia katika ndoa wakati hata maumbile yake bado ni madogo, hata kura hawezi kupiga lakini anakuwa mke wa mtu,” anasema

Anasema zaidi jinsi Katiba Inayopendekezwa ilivyoyafanyia kazi maoni yao yaliyohusu haki za wanawake na kusema kwa sasa kuna marekebisho ya sheria ya kimila ambayo katiba ya zamani haikumtambua mtoto wa kike kama mrithi wa mali isiyohamishika jambo ambalo kwa sasa halipo.

Aidha, anasema sheria nyingi zilizokuwapo katika katiba ya zamani zilionekana kukinzana. Kwa mfano, sheria hizo hazikufafanua mtoto ni nani na ana haki gani na kwa upande mwingine zikiruhusu mtoto kufunga ndoa.

“Tulitumia fursa hii vyema kwa sababu tulijua kabisa katiba ni moyo na ikitengenezwa basi kuibadili huwa ni kazi vigumu lakini tunashukuru maoni yetu yalifanyiwa kazi,” anasema

Katika kuhakikisha wanatoa maoni bora ya katiba, Tawla walitembelea nchi za Afrika Mashariki ili kujifunza jinsi ambavyo nchi hizo ziliunda katiba yenye manufaa hasa kwa upande wa haki za kijinsia.

“Tulijifunza kwa kina kabla ya kutoa maoni yetu, hatukutembea Afrika Mashariki tu, bali tulifika hata Afrika Kusini nia ilikuwa ni kuhakikisha mwanamke anatambulika na anakuwa na fursa katika katiba hii,” anasema.

Mwanasheria, Cecilia Assey anawaasa wanawake kuacha woga pindi wanapokumbana na unyanyasaji kutoka kwa waume, wenza au wanajamii kwani sheria zipo.

“Hapa tunapata elimu kuhusu katiba na masuala ya jinsia lakini baada ya mafunzo haya tutaendelea na kazi ya kuwasaidia wanawake wanaokumbana na changamoto katika jamii,” anasema.

Chanzo: Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una