Skip to main content

Tarime watoto zaidi ya 600 wakimbia kukeketwa wilayani Tarime


Click image for larger version. 

Name: IMG_0078_0.JPG 
Views: 0 
Size: 80.2 KB 
ID: 212145

Ukifika nje ya geti la Kituo cha Masanga tangu mwezi huu wa 12 ulipoanza utakutana na huu ujumbe ''HAKATWI MTU HAPA'' hiki ni kituo cha kuzuia ukeketaji (TFGM) ambacho kinatoa mafunzo ya ukeketaji mbadala na tohara salama... kwa sasa kuna watoto zaidi ya 600 ambao wamekimbilia hapa ili wasikeketwe tangu msimu huu ulipoanza mwezi wa 12/2014...

Mwezi wa 12 ni mwezi wa kufanya tohara mkoani Mara ambapo watoto wengi huwa wamefunga shule na hivyo kupelekea watoto wa kike hukeketwa...






Click image for larger version. 

Name: IMG_0269_3-1.JPG 
Views: 0 
Size: 64.1 KB 
ID: 212146

Mabango haya yamebeba ujumbe tofautitofauti kwa lengo la kuifikishia jamii kilio chao kutokana na hii mila yao ya Ukeketaji...


Click image for larger version. 

Name: MSAADA TARIME(4).jpg 
Views: 0 
Size: 66.9 KB 
ID: 212138

Nimeona ni busara kuwaomba Umma tushirikiane kuwasaidia watoto hawa hasa kipindi hiki kigumu ambacho wamekimbia kukeketwa wakingojea msimu uishe mwezi huu wa 12 warudi makwao wakaendelee na shule... yaani hawana hata maji! kama ujuavyo maji ni muhimu sana kwa binadamu, na huwa wanategemea maji ya mvua!!! sasa mvua hazijanyesha hivi karibuni... pia hawana chakula, pedi, nguo, viatu, kama una maswali zaidi unaweza kumuuliza mkuu wa kituo hicho Sister Germana... Lakini chondechonde nakuomba tuwasaidie wako kwenye hali mbaya...

Habari hii nimeitoa www.wanawakelivetv.com

Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa...

SOMO LA KWANZA : UTENGENEZAJI WA SABUNI ZA AINA ZOTE.

 MASOMO  YATAKAYO  FUNDISHWA  HAPA  NI : 1 1. Utengenezaji  Wa Sabuni  isiyo na garama. 22. Utengenezaji  Wa Sabuni ya urembo. 33. Utengenezaji  Wa  Sabuni ya asali na cream. 4 4.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya manukato. 5 5.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ngumu. 66.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya unga 77. Utengenezaji   Wa Sabuni ya kugandisha. 8 8. Utengenezaji    Wa  Sabuni za dawa. 99. Utengenezaji  Wa  Sabuni za rangi. 110.  Utengenezaji  Wa Cream ya kunyolea. 111. Utengenezaji  Wa  Sabuni iliyotengenezwa na mafuta mengine.  VIFAA     VYA     UTENGENEZAJI   SABUNI. *Sufuria. *Bakuli kubwa la mfinyanzi au plastiki. *Mafuta *Maji. *Sodium hydroxide{NaOH} *Ubao mdogo/mwiko.  *Chombo chenye ukubwa cha plastiki. *Kifyatulio. *Ki...

SOMO LA TISA : USINDIKAJI WA MAZAO YA NAFAKA

Mahindi  yaliyo  toka  kuvunwa. 1 .   USINDIKAJI  WA   ZAO  LA  MAHINDI : Ili kuongeza matumizi ya mazao hayo na kudumisha ubora wake ni muhimu teknolojia za kusindika nafaka zitumike. Usindikaji pia huongeza thamani ya zao.                             KUSINDIKA MAHINDI Punje za mahindi hutumika kupika makande na husindikwa kupata unga unaotumika katika matumizi mbalimbali. Vile vile bidhaa nyingine zinazotokana na mahindi ni mafuta na wanga. KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA Kuna aina mbili za unga wa mahindi, unga wa mahindi yasiyokobolewa(Dona) na unga wa mahindi yaliyokobolewa (Sembe)  KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA WA DONA Vifaa • Mashine ya kukoboa • Mashine ya kusaga • Ungo • Debe • Mifuko • Chekeche ya nafaka Jinsi ya kusindika • Pepeta na pembua mahindi ili kuondoa vumbi na takataka nyingine kwa kutumia chekeche, ungo a...