Skip to main content

NAFASI ZA KAZI ( FOOD PRODUCTION)

NAFASI   ZA KAZI   ( FOOD PRODUCTION )


 


RafikiElimu  Education Consultancy ni Taasisi inayo jihusisha na usimamizi wa maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi wanao soma katika shule za msingi na sekondari nchini Tanzania, pamoja  na mafunzo ya ujasiriamali. Taasisi  Kwa kushirikiana  na shule mbalimbali za msingi na sekondari katika mikoa ya Dar Es Salaam na Mtwara   inaratibu  mradi wa “ MAFUNZO YA UTENGENEZAJI  WA PIPI ZA VIJITI” almaarufu kama “ PIPI ZA KIHINDI”, kwa vijana waliomaliza kidato cha nne.   Lengo  la mafunzo haya ni kuwajengea   vijana hao , uwezo wa kujiajiri wenyewe  kwa kutengeneza  na kuuza pipi hizo kwenye shule za msingi na sekondari ambazo zinashirikiana na taasisi  katika mradi huu.   Kupitia mradi huu, taasisi inatangaza  nafasi za kazi  ya  kufundisha namna ya kuandaa na kutayarisha pipi za vijiti ( Pipi za kihindi ). Mafunzo haya  yatatolewa kwa vijana  wanao simamiwa na taasisi yetu katika mradi huu.

SIFA ZA MWOMBAJI NAFASI :

1.       Awe na elimu ya kuanzia ngazi ya cheti katika fani ya FOOD PRODUCTION kutoka katika chuo kinacho tambuliwa na serikali  au AWE  Mwanafunzi anae chukua kozi ya FOOD PRODUCTION kuanzia ngazi ya cheti na kuendelea.

2.       Awe wa jinsia yoyote  mwenye  uwezo mkubwa wa kujielezea na kuelekeza.

3.       Awe maridadi,mwaminifu, mwenye bidii na nidhamu.

IDADI YA  NAFASI :  idadi ya nafasi za kazi zilizopo kwenye mradi huu ni nafasi kumi na saba ( 17)

MUDA WA MRADI : Mradi huu utafanyika kwa muda wa miezi  sita kuanzia tarehe 02 DESEMBA 2024.

MAJUKUMU YA KAZI : Majukumu ya kazi kwa watakao fanikiwa kupata nafasi hii yatakuwa ni kutoa mafunzo ya jinsi ya kutengeneza pipi za vijiti, pamoja na kuwasimamia wahitimu wa mafunzo hayo kwenye vituo vyao vya kazi.( Mashuleni )

Waombaji watakao pata nafasi hii ya kazi watapewa semina maalumu itakayo wajengea uwezo wa kufanya kazi katika mradi huu kama wakufunzi wa mafunzo ya kutengeneza pipi za vijiti.

JINSI YA KUTUMA MAOMBI:  Maombi yote yatumwe kupitia barua pepe yetu ambayo ni: rafikielimutanzania@gmail.com.  Maombi yote yaambatanishwe na CV pamoja na passport size ya rangi.

MWISHO WA  KUTUMA MAOMBI : Mwisho wa kutuma maombi haya ni tarehe 31 OCTOBER 2024.

Kwa maelezo zaidi:  Tutembelee kupitia tovuti yetu : www.rafikielimu.blogspot.com

 


Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una 

SOMO LA KWANZA : UTENGENEZAJI WA SABUNI ZA AINA ZOTE.

 MASOMO  YATAKAYO  FUNDISHWA  HAPA  NI : 1 1. Utengenezaji  Wa Sabuni  isiyo na garama. 22. Utengenezaji  Wa Sabuni ya urembo. 33. Utengenezaji  Wa  Sabuni ya asali na cream. 4 4.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya manukato. 5 5.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ngumu. 66.  Utengenezaji   Wa  Sabuni ya unga 77. Utengenezaji   Wa Sabuni ya kugandisha. 8 8. Utengenezaji    Wa  Sabuni za dawa. 99. Utengenezaji  Wa  Sabuni za rangi. 110.  Utengenezaji  Wa Cream ya kunyolea. 111. Utengenezaji  Wa  Sabuni iliyotengenezwa na mafuta mengine.  VIFAA     VYA     UTENGENEZAJI   SABUNI. *Sufuria. *Bakuli kubwa la mfinyanzi au plastiki. *Mafuta *Maji. *Sodium hydroxide{NaOH} *Ubao mdogo/mwiko.  *Chombo chenye ukubwa cha plastiki. *Kifyatulio. *Kisu. *Vikombe 2 vya plasitiki. * Makopo  2  ya plasiki au kaure. Vipimo vinavyo tajwa hapa ni chombo chochote cha plastic ( kama kikombe,kopo n.k.} Vipimo vyote ni vya ujazo na mara zote vikae wi