Skip to main content

NAFASI ZA MAFUNZO YA UTENGENEZAJI MASHINE ZA KUTOTOLEA VIFARANGA WA KUKU ( INCUBATORS)







Taasisi  ya  RafikiElimu  FOUNDATION  kupitia  MRADI  WA  ELIMU  YA  UJASIRIAMALI  MIJINI  NA  VIJIJINJI  inatangaza  nafasi  za   MAFUNZO  YA  UTENGENEZAJI  WA  MASHINE  ZA  KUTOTOLEA  VIFARANGA  WA  KUKU.

Mashine   zitakazo fundishwa  kutengeneza  ni  INCUBATOR   ( MANUAL & AUTOMATIC) ZENYE  UWEZO  WA  KUTUNZA  JOTO  KWA  SAA  48 PAMOJA  NA  KUTOTORESHA  MAYAI   KUANZIA  240  HADI  5000.






ADA   YA   MAFUNZO   :

Ada  ya  mafunzo  haya  ni  SHILINGI  LAKI  MBILI  NA  ELFU  HAMSINI  TU  (Tshs. 250,000/=)  na  inalipwa  kwa  awamu mbili.

TAREHE  YA  KUANZA  KWA  MAFUNZO

Mafunzo  haya  yatafanyika  kwa  muda   mwezi  mmoja  kuanzia  tarehe    06   OKTOBA  2014  hadi  tarehe  10  NOVEMBA  2014.


FOMU   ZA   KUJIUNGA   NA   MAFUNZO :

Fomu  za  kujiunga  na  mafunzo  haya  zinapatikana  ofisini  kwetu  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  KUMI  NA  TANO  TU  ( Tshs.15,000/=).

MWISHO  WA  KUCHUKUA  FOMU  :

Mwisho  wa  kuchukua  fomu  ni  tarehe   30  SEPTEMBA  2014.

Ofisi  zetu  zinapatikana  katika  eneo  la  CHANGANYIKENI  karibu  na  CHUO  CHA  TAKWIMU.

JINSI   YA   KUFIKA   OFISINI   KWETU:

Kufika  ofisini  kwetu, panda  daladala za  UBUNGO- CHANGANYIKENI  kisha  shuka  kituo  cha  TAKWIMU  halafu  tembea  hatua  ishirini  mbele  kisha  tazama  upande  wako  wa  kulia utaona  ofisi  imeandikwa   RAEFO  TANZANIA.
Kwa  maelezo  zaidi  wasiliana  nasi  kwa  simu 0784406508.

KWA   WAOMBAJI   WALIOPO  NJE  YA  MKOA  WA  DAR  ES  SALAAM:
Kwa  waombaji  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  salaam,, mafunzo  yatatolewa  kwa  njia ya  posta.

JINSI  YA  KUTUMA  MAOMBI  KWA  WAOMBAJI  WALIOPO  NJE  YA  MKOA  WA  DAR  ES  SALAAM.


Kwa  waombaji  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  salaam, watatumiwa  fomu  za  kujiunga  na  mafunzo  haya  kwa  njia  ya  barua  pepe.  Tuma  barua  pepe  ya  maombi  ya  fomu  ya  kujiunga  na  mafunzo  haya  kupitia  barua  pepe  yetu  ambayo  ni : rafikielimutanzania@gmail.com .
Maombi yako  yaelekezwe  kwa  Mkurugenzi  Mtendaji, RafikiElimu  Foundation.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tafadhali  tembelea :

Au tembelea  :   www.rafikielimu.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una