Skip to main content

Posts

Showing posts from 2014

Asilimia 97 kujiunga kidato cha Kwanza 2015

Wanafunzi  wa  shule  ya  sekondari. Jumla ya wanafunzi 438,960 kati ya wanafunzi 451,392 waliofaulu mtihani wa darasa la saba nchini Tanzania wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za serikali za sekondari kwa awamu ya kwanza. 0 Mhe. Majaliwa Kasim Majaliwa Akitangaza matokeo ya ufaulu huo kwa vyombo vya habari na wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Mhe. Majaliwa Kasim Majaliwa amesema idadi hiyo ni sawa na asilimia 97.23 ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo. Naibu waziri, Majaliwa amesema kati ya wanafunzi waliochaguliwa wasichana ni 219,996 sawa na asilimia 97.1 na wavulana 218964 sawa na asilimia 97.28 na kuongeza kuwa takwimu h

Tawla: Wanaume mnaopigwa na wake zenu jitokezeni

Ni nadra kusikia mwanamume akilalamika kuwa amepigwa na mke au mwenza wake. Suala hilo ni adimu zaidi katika nchi za Afrika hasa zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara ambazo zimefunikwa na blanketi la mfumo dume. Kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni woga, aibu na kasumba ya mfumo dume, wanaume wanaonyanyaswa wamekuwa wakificha aibu hiyo na kuendelea kubaki katika unyanyasaji huo. Kutokana na ongezeko la matukio ya wanaume kunyanyaswa na wake au wenza, Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania, (Tawla) kimetoa wito kwa wanaume kujitokeza ili kupata msaada wa kisheria pindi wanaponyanyaswa. Mwenyekiti wa asasi zisizo za kiserikali za katiba na jinsia, (Zec) zinazoratibiwa na Tawla, Victoria Mandari anasema matukio hayo ni mengi lakini wanaume wamekuwa wakiyafanya kuwa siri pengine kwa kuona aibu. “Wanaume watafute chama kitakachowasaidia kutetea haki zao na kutengeneza hata sheria ambazo zitawasaidia kupata haki zao,” anasema. Anasema sheria zinasema kuw

Tarime watoto zaidi ya 600 wakimbia kukeketwa wilayani Tarime

Ukifika nje ya geti la Kituo cha Masanga tangu mwezi huu wa 12 ulipoanza utakutana na huu ujumbe ''HAKATWI MTU HAPA'' hiki ni kituo cha kuzuia ukeketaji (TFGM) ambacho kinatoa mafunzo ya ukeketaji mbadala na tohara salama... kwa sasa kuna watoto zaidi ya 600 ambao wamekimbilia hapa ili wasikeketwe tangu msimu huu ulipoanza mwezi wa 12/2014... Mwezi wa 12 ni mwezi wa kufanya tohara mkoani Mara ambapo watoto wengi huwa wamefunga shule na hivyo kupelekea watoto wa kike hukeketwa... Mabango haya yamebeba ujumbe tofautitofauti kwa lengo la kuifikishia jamii kilio chao kutokana na hii mila yao ya Ukeketaji... Nimeona ni busara kuwaomba Umma tushirikiane kuwasaidia watoto hawa hasa kipindi hiki kigumu ambacho wamekimbia kukeketwa wakingojea msimu uishe mwezi huu wa 12 warudi makwao wakaendelee na shule... yaani hawana hata maji! kama ujuavyo maji ni muhimu sana kwa binadamu, na huwa wanategemea maji ya mvua!!! sasa mvua hazijanye

Kutoka ndoto ya kuwa mtafiti hadi kuwa DG wa Taasisi ya Utafiti (NIMR Tanzania)

A PERSONAL JOURNEY: FROM PARASITE IMMUNOLOGY TO DISEASE CONTROL. MWELECELE MALECELA My career at NIMR is a true story of serendipity rather than design. I joined NIMR in 1987 after graduating form the University of Dar-es-Salaam with a B.Sc. in Zoology in 1986. After an extremely rigorous interview process I was assigned to work at the Amani Center and to specifically focus on a disease they called Bancroftian Filariasis. Now I had heard of this disease in my classes at UDSM and the great tutelage of Dr Parkin but I had know idea what I was going to do. In my mind I wanted to work on malaria which at the time I thought was more interesting area of research. So I must say I was quite depressed as at the time Malaria research had the most resources in terms of funding and equipment. I was told explicitly that I was to work to revive the Bancroftian filariasis work at Amani. As one who always thrives on a ch

Ngono zembe yatawala hiki kijiji, ina maana hawaogopi UKIMWI

Hii ndio hali halisi utakayo kutana nayo kilometa 660 kutoka Dar es Salaam na kilimeta 122 kutoka Nachingwea. Katika kijiji cha Kiegei kila tarehe 25 ya mwisho wa mwezi, baada ya mnada wa bidhaa mbalimbali za kilimo kama chakula na vifaa vya nyumbani kama vyombo. Watu wengine, wekiwemo watoto wa shule za msingi huuziana mabusu na wafanyabiashara wa mnada huo, kusababisha kukatisha masomo kwa baadhi ya wanafunzi kwa kushika ujauzito na wengine kupata magonjwa ya kuambukiza kama gono, kaswende na Ukimwi. Baada ya kuuza bishaa zao mbalimbali katika mnada huo, unaohusisha wafanyabiashara kutoka katika wilaya za jirani kama Liwale, Tunduru na Masasi, wafanyabiasha wa Kiegei huingia katika vibanda vya sinema, mathalani kuangalia filamu mbalimbali, lakini humo ndani ya vibanda filamu hutumia pesa zao kununua ngono kutoka kwa watoto. Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 inalenga kuhakikisha kwamba watoto wote wanastawi na kuwa na maisha bora,

NAFASI ZA MAFUNZO YA UTENGENEZAJI MASHINE ZA KUTOTOLEA VIFARANGA WA KUKU ( INCUBATORS)

Taasisi   ya   RafikiElimu   FOUNDATION   kupitia   MRADI   WA   ELIMU   YA   UJASIRIAMALI   MIJINI   NA   VIJIJINJI   inatangaza   nafasi   za    MAFUNZO   YA   UTENGENEZAJI   WA   MASHINE   ZA   KUTOTOLEA   VIFARANGA   WA   KUKU. Mashine    zitakazo fundishwa   kutengeneza   ni   INCUBATOR    ( MANUAL & AUTOMATIC) ZENYE   UWEZO   WA   KUTUNZA   JOTO   KWA   SAA   48 PAMOJA   NA   KUTOTORESHA   MAYAI    KUANZIA   240   HADI   5000. ADA    YA    MAFUNZO    : Ada   ya   mafunzo   haya   ni   SHILINGI   LAKI   MBILI   NA   ELFU   HAMSINI   TU   (Tshs. 250,000/=)   na   inalipwa   kwa   awamu mbili. TAREHE   YA   KUANZA   KWA   MAFUNZO Mafunzo   haya   yatafanyika   kwa   muda     mwezi   mmoja   kuanzia   tarehe      06    OKTOBA   2014   hadi   tarehe   10   NOVEMBA   2014. FOMU    ZA    KUJIUNGA    NA    MAFUNZO : Fomu   za   kujiunga   na   mafunzo   haya   zinapatikana   ofisini   kwetu   kwa   gharama   ya   SHILINGI   ELF