Skip to main content

SULUHISHO LA CHANGAMOTO ZINAZO WAKABILI WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO TANZANIA



Mradi  wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  na  Vijijini “ EUMIVI  PROJECT” ni  mradi  unao  ratibiwa  na  Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation  kwa  kushirikiana  na  mashirika  rafiki.   Mradi  huu  ulizinduliwa  rasmi   tarehe  01  Septemba  2012  jijini  Dar  Es  salaam na  kuwahusisha  wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  jijini  Dar  Es  salaam  ambao  walipewa   mafunzo  ya  utengenezaji  wa  bidhaa  mbalimbali  kama  vile  sabuni  za  aina  zote, chaki  na  mishumaa  kwa  kutaja  vichache.  Baada  ya  hapo  mafunzo  yalielekea  katika  jiji  la  Arusha  ambapo  wajasiriamali  mbalimbali  wa  jijini  Arusha  walipatiwa  mafunzo  ya  utengenezaji  wa  bidhaa  mbalimbali.

Mafunzo  haya  yalifanyika  pamoja utafiti  uliokuwa  ukifanywa  na  taasisi  hii  kuhusu  changamoto  mbalimbali  zinazo  wahusu wajasiriamali  wadogo  nchini  Tanzania. Utafiti  huo  wenye  kichwa  “ CHANGOMOTO  ZINAZOWAKABILI  WAJASIRIAMALI  WADOGO  WADOGO  NCHINI  TANZANIA”    uligundua  mambo  yafuatayo  kama  changamoto  hizo. Mambo  hayo  ni  pamoja  na : 


1.      Ukosefu  wa  waalimu  wa  Ujasiriamali :  Utafiti  wetu  umetuwezesha  kugundua  kuwa  Tanzania  ni  miongoni  mwa  nchi  za   Afrika  zinazo  kabiliwa  na  tatizo la  ukosefu  wa  waalimu wa  kutosha  wa  somo  la  ujasiriamali. Suala  hili  lilitugharimu  sana  hata  sisi  kama  taasisi  katika  awamu  ya  kwanza  ya  mafunzo  ya  mradi  huu.
2.       Ukosefu  wa   Elimu  Ya  Uhakika  Ya  Ujasiriamali:  Hapa  ninazungumzia   elimu  ya  namna  ya  kufanya  ujasiriamali. Wajasiriamali  wengi  wadogo  wadogo  wa  hapa  Tanzania  hawana  elimu  ya  kutosha  ya  ujasiriamali, elimu  inayo  weza  kuwasaidia  kufanya  ujasiriamali  kwa  mafanikio  makubwa.  Hii  inatokana  na  ukosefu  wa waalimu  wa  ujasiriamali  Tanzania.

3. Ukosefu  wa  Elimu  Uhakika  Ya  Utengenezaji  wa  Bidhaa  Mbalimbali : Utafiti  wetu  umegundua  kuwa  wajasiriamali wengi  wadogo wadogo  wa  hapa  Tanzania, hawana  elimu  ya  kutosha  juu  ya  utengenezaji  na  uzalishaji  wa  bidhaa  mbalimbali  kama  vile  sabuni,  mishumaa, chaki  nakadhalika.. Endapo  wajasiriamali  wakipewa  ujuzi  kuhusu  utengenezaji  wa  bidhaa  mbalimbali, ujuzi  huo  unaweza  kuwasaidia  kuongeza  wigo  wa  shughuli  zao  za  kijasiriamali, kwa  mfano  mjasiriamali  ambaye  alikuwa  hajui  kutengeneza  losheni, akipewa  elimu  kuhusu  utengenezaji  wa  losheni  maana  yake atakuwa  na  uwezo kujiongezea  kipato  zaidi  kupitia  utengenezaji  wa  losheni.

4. Kuwa  na  ujuzi  wa  utengenezaji  wa  bidhaa zinazo  fanana :  Kwa  mujibu  wa  utafiti  wetu, wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  Tanzania  wana  ujuzi  wa  utengenezaji  wa  bidhaa  zinazo  fanana.  Bidhaa  zinazo  tengenezwa  na  wajasiriamali  wengi  wa  Tanzania  ni  sabuni  za  maji, pamoja  na   mango pickle na  Tomato Sauce  kwa  kzitaja  chache.  Hata  hivyo, ujuzi  huu  hauwasaidii  sana  wajasiraiamali  hawa  kwa  sababu  karibu  kila  mtu  anaye  fanya  ujasiriamali  anafahamu  kuhusu  utengenezaji  wa  bidhaa  hizo  hizo  tu, so  linapo  kuja  suala  la kuudha  bidhaa  zao,jambo  hili  linasimama  kama  changamoto.

5. Kutokuwa  na  uwezo  wa  kutengeneza  bidhaa  zenye  ubora :  Utafiti  wetu  umetuwezesha  kugundua  kuwa wajasiriamali  wengi  wadogo  wadogo  wa  Tanzania, hawana  uwezo  wa  kutengeneza  bidhaa  zenye  ubora  unaoweza  kutoa  ushindani  wa  kibiashara  kwa  wajasiriamali wa  kati  na  wakubwa  ambao  nao pia  wanajihusisha  na  utengenezaji  wa  bidhaa  hizo  hizo.  Hali  hii  imewafanya  wajasiriamali wengi  wadogo  wadogo  wa  Tanzania  kushindwa  kuendeleza  biashara  zao  kwa  sababu  ya  kutengeneza  bidhaa  zisizokuwa  na  kiwango  kinacho  kidhi  ushindani.

6. Kutokuwa  na  sifa /uwezo  wa  kupata  mikopo  kwenye  taasisi  za  kifedha : Wajasiriamali  wengi  wadogo  wadogo hapa  nchini  Tanzania  wana mawazo  mazuri  ya  kibiashara  na  wengine  wana  elimu  ya  msingi  kuhusu  utengenezaji wa  bidhaa  mbalimbali  lakini  wanashindwa  kuyaweka  mawazo  na  ujuzi  wao  katika  vitendo  kwa  sababu  ya  kutokuwa  na  mitaji  ya  kuanzisha  biashara  na  kwa  wale  ambao  tayari wamekwisha  anza  biashara,  wanashindwa  kupata  pesa  zaidi  kwa  ajili  ya  kuendeleza  biashara  zao. Moja  kati  ya  sababu  zinazo  wafanya  wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa   Tanzania  kushindwa  kupata  mikopo  kutoka  katika  taasisi  mbalimbali  za  kifedha  ni   pamoja  na  kutokukidhi  sifa  za  kukopeshwa  lakini  pili  kutokujua  taratibu  za  kuomba  mikopo.

7. Kutokuwa  na   chombo  maalumu  kw  ajili  ya  kutangaza  shughuli  za   wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  Tanzania.

8.  Kutofahamu  sheria  na  taratibu  za  uanzishaji  na  uendelezaji  wa  biashara  na  kampuni.

9.  Ukosefu  wa  vifungashio  vinavyo  kidhi  matakwa ya  bidhaa  mbalimbali.

10. Ukosefu  wa  malighafi  za  utengenezaji  wa  bidhaa  mbalimbali  kama  vile  sabuni, mishumaa, chaki, losheni, mafuta  ya  kujipaka, pafyumu  nakadhalika.


SULUHISHO   LA   CHANGAMOTO  ZINAZO  WAKABILI  WAJASIRIAMALI  WADOGO  WADOGO  WA  TANZANIA
Kufuatia  changamoto  hizo  hapo  juu, Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation  kwa  kushirikiana  na  mashirika  rafiki  imeamua  kufanya  mambo  yafuatayo  kwa  ajili  ya  kukabiliana na  changamoto  hizo:


1.    Kuanzisha  mafunzo  ya  Ualimu  wa  Ujasiriamali:  Taasisi  ya  RafikiElimu  imeamua  kuanzisha  mafunzo  ya   UALIMU  WA  UJASIRIAMALI kwa  vijana  mbalimbali  wa  kitanzania. Mafunzo  haya  yatasaidia  katika  kuwaandaa  vijana  mbalimbali  wa  kitanzania  kuwa  waalimu  wa  ujasiriamali  na  hivyo  kupunguza  tatizo  la  ukosefu  wa  waalimu  wa  ujasiriamali.  Taasisi  imepanga  kuwafundisha  vijana  wapato  mia  moja  ( 100)  katika  kila  wilaya  ya  Tanzania  bara  kama  waalimu  wa  ujasiriamali.

2.       Kuanzisha  MTANDAO  WA  WAALIMU  WA  UJASIRIAMALI  TANZANIA :  Mtandao  huu  utawahusisha  vijana  walio  hitimu  mafunzo  ya  ualimu  wa  ujasiriamali, na  utafanya  kazi  na  kuwa  na  ofisi  katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara. Mtandao  utahusika  na  kuratibu  shughuli  zote  za  mradi  katika  wilaya  husika  kama  vile  kusimamia  utolewaji  wa  mafunzo  ya  ujasiriamali .

3.      Kuanzisha  vituo  vya  mafunzo  ya  ujasiriamali  katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara. Vituo  hivi  vitahusika  na  kutoa  mafunzo  ya  ujasiriamali  kwa wajasiriamali  wadogo  wadogo  kwenye  wilaya  zote  za  Tanzania  bara. Vituo  hivi  vitasimamiwa  na  ofisi  ya  mtandao  wa  waalimu  wa  ujasiriamali  katika  wilaya  husika.

4.      Kuanzisha  vikundi  vya  kuweka  na  kukopa  SACCOSS” pamoja  na   VICOBA  katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara.Vikundi  hivi  vitawahusisha  waalimu  wa  ujasiriamali  pamoja  na  wajasiriamali  wadogo  wadogo  watakao  jiunga  na  mafunzo  yetu  na  vitafanya  kazi  katika  malengo  ya  kuwa  benki  ya  kijamii “ Community  Bank “

5.      Kuanzisha  jarida  maalumu  litakalo  husika  na  kutangaza  bidhaa  na  shughuli  za  wajasiriamali wadogo  wadogo  waliopitia  mafunzo  yetu. Jarida  hilo  litaitwa  “ MJASIRIAMALI” na  litasambazwa   katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara. Jarida  hili  litawasaidia  sana  wajasiriamali wadogo  wadogo  kutangaza  biashara  zao.

6.      Kuanzisha  maonyesho   madogo  madogo  ya  biashara   yatakayo  husu  bidhaa  za  wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  Tanzania  bara.

7.      Kuanzisha  mashindano  na  tuzo  mbalimbali  yatakayo  wahusisha  wajasiriamali  wadogo wadogo  wa  Tanzania  bara. Mfano: mashindano  ya  kushindanisha  ubora  wa  bidhaa  za  wajasiriamali  wadogo  wadogo. Tuzo  hizi  zitachangia  katika  kuzitangaza  bidhaa  za  wajasiriamali husika  lakini  pia  zitasaidia  katika kuongeza  ari  na  ufanisi  kwa  wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  Tanzania  bara.

8.      Kushirikiana   na  wajasiriamali  wa  nje  ya  Tanzania  kufanya  maonyesho  ya  wajasiriamali  wadogo  wadogo  ili  kusaidia  kuzitangaza  biashara  na  shuguli za  wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  Tanzania  bara.

9.      Kuanzisha  duka   la  kuuza  malighafi  zinazo  tumika  katika  kutengeneza  bidhaa  mbalimbali  kama  vile  mafuta  ya  kujipaka, losheni  na  pafyumu. Malighafi  hizo  zitauzwa  kwa  bei  nafuu  na  zitasambazwa  katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara.

10.  Kuanzisha  duka  la  kuuza  vifungashio  kwa  wajasiriamali  wadogo  wadogo  wa  Tanzania  bara.
11.  Lengo   la  Mradi : 

Lengo  la  mradi  huu  ni  kuwatrain  walimu  wa  ujasiriamali  wapatao  mia  moja  katika  kila  wilaya  ya  Tanzania  Bara na  kisha  kuwatumia  kuunda  MTANDAO  WA  WAALIMU  WA  UJASIRIAMALI  TANZANIA,  utakao  husika  na  kutoa  mafunzo  ya  ujasiriamali  kwa  wajasiriamali  wadogo  wadogo  waliopo  katika  wilaya  wanazo  ishi .

        MAFUNZO   YATAKAYO   TOLEWA   :
   Mafunzo  yatakayo  tolewa   kwa  wanafunzi  wa  ualimu wa  ujasiriamali  katika  mradi  huu  ni  pamoja  na  utengenezaji & uzalishaji  wa  bidhaa  mbalimbali  kama  vile  sabuni, mishumaa, chaki, maji ya  betri, manukato ( perfume ), losheni, mafuta  ya  kujipaka, usindikaji  wa  vyakula, usindikaji  wa  bidhaa  za  ngozi  kama  vile  viatu, mikanda  na  mabegi.  Uanzishaji & uendelezaji wa  taasisi  zisizokuwa  za  kiserikali ( NGO  Management & Operation ),uanzishaji wa  kampuni  za  kibiashara, uanzishaji  wa  SACCOSS na  VICOBA  nakadhalika.

UTARATIBU   WA   MAFUNZO   KWA   WAALIMU  WA  UJASIRIAMALI

Mafunzo  haya  yatatolewa  kwa  awamu  mbili, awamu ya  kwanza  itakuwa  ni  kwa  wakaazi  wa  Dar  Es  salaam, ambayo  itaanza  tarehe  01  Agosti  2013  hadi  tarehe  20   Agosti  2013, na  awamu  ya  pili  ya  mafunzo  itaanza  tarehe  01  Septemba  2013 hadi  tarehe    20  Septemba  2013  na  yata  wahusisha  wakaazi  wa  mikoa  mingine  iliyo  baki.

MAFUNZO   YA   DAR   ES   SALAAM.
Mafunzo  ya  Dar  Es  salaam yataanza  tarehe  01  AGOSTI  2013  na  yatafanyika  katika  Chuo  Kikuu  Cha  Dar  Es  salaam , ( SEHEMU  YA  MLIMANI )

MAFUNZO   YA   NJE   YA   DAR   ES  SALAAM.

Mafunzo  yatakayo  fanyika  nje  ya   mkoa  wa  Dar  Es  slaam  yatafanyika  kuanzia  tarehe  01  SEPTEMBA  ambapo  wanafunzi  wa  ualimu  wa  ujasiriamali  watakao  hitimu  katika  mafunzo  ya  Dar  Es  salaam,  watatembelea  wilaya  tofauti  tofauti  za  Tanzania  bara  kwa  ajili  ya  kutoa  mafunzo  hayo  kwa  wanafunzi  wa  mafunzo  haya  waliopo  mikoani.

BAADA   YA   KUHITIMU   MAFUNZO
Baada  ya  kuhitimu  mafunzo  haya  wahitimu  wote  wataunda  mtandao  wa  waalimu  wa  ujasiriamali  nchini  Tanzania  ambao  utafanya  kazi  katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara.   Mtandao  utahusika  na  kuanzisha  vituo  vya  ujasiriamali  katika  wilaya  zote  za  Tanzania  bara. Vituo  hivi  vitahusika  na  kutoa  mafunzo  ya  ujasiriamali  kwa  bei  nafuu  kwa  wajasiriamali  wadogo  wadogo  waliopo  katika  wilaya  husika.
Hii  ni  nafasi  nzuri  kwa  vijana  wa  kitanzania  wasio  kuwa  na  ajira, kuweza  kujiajiri  kupitia  mradi  huu.

ADA  YA  MAFUNZO:  Ada  ya  mafunzo  haya  ni  Shilingi  Elfu  Sitini  na  Tano  tu  za  Kitanzania  ( Tshs.65,000/=).

FOMU  ZA  KUJIUNGA  NA  MAFUNZO  HAYA :  Fomu  za  kujiunga  na  mafunzo  haya  zinapatikana  kwa  shilingi  Elfu  Kumi  na  Mbili  Tu ( Tshs.12,000/=)  katika  ofisi  zetu  zilizopo  katika  eneo  la  CHANGANYIKENI  karibu  na  Chuo  Cha  Takwimu.
  Mwisho  wa  kuchukua  fomu  za  kujiunga  na  Mafunzo  Haya: Mwisho  wa  kuchukua  fomu  za  kujiunga  na  mafunzo  haya  ni  tarehe   25  Julai  2013. Mafunzo  yataanza  tarehe  01  AGOSTI  2013.

Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una