Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2013

MAFUNZO YA KUTENGENEZA LOSHENI, MAFUTA YA KUJIPAKA NA PAFYUMU..

Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, inapenda  kuwatangazia   vijana  wote  wa  kitanzania, nafasi  za   kushiriki  katika  mafunzo  ya  utengenezaji  wa  bidhaa  mbalimbali.  Bidhaa  zitakazo  fundishwa  ni  pamoja  na   UTENGENEZAJI  WA  MAFUTA  YA  KUJIPAKA , LOSHENI   na  MANUKATO. SIFA  ZA  WASHIRIKI :  Mtu  Yoyote  anaweza  kushiriki  katika  mafunzo  haya. ADA  YA  KUSHIRIKI   :  Ada  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  ni  Shilingi  ELFU  ISHIRINI  NA  TANO  TU ( Tshs. 25,000/= ). Mafunzo  yatafanyika  kwa  muda  wa  siku  tatu  kuanzia  tarehe   01  AGOSTI  2013   hadi  tarehe  03  AGOSTI  2013.  MAHALI  :  Mafunzo  haya  yatafanyika  katika  Chuo  kikuu  cha  Dar  Es  salaam. Mwisho  wa  kujiandikisha  ni  tarehe  28  JULAI  2013. WAHI  KUJIANDIKISHA  MAPEMA, KWANI  NAFASI  ZILIZOPO  NI  CHACHE.  

NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU WA UJASIRIAMALI.

Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation  inatangaza    nafasi  za  mafunzo  ya   UALIMU   WA   UJASIRIAMALI   kwa   waombaji   wenye   sifa   zifuatazo ; 1.    Mtanzania    mwenye  umri  wa  kuanzia  miaka  18  hadi  45. 2.Awe   na  elimu  ya  kuanzia  kidato  cha   nne,  sita  na  kuendelea.  3. Aliye   na   utashi  na malengo  ya  kufanya kazi    kama  MWALIMU  WA  UJASIRIAMALI  kwenye  Mradi  Wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini. 4. Anayeweza    kuwasiliana   kwa    ufasaha   kwa   lugha   za   Kiswahili   na   kiingereza. 5.  Awe  anaishi    katika    wilaya   ya   Ilala, Kinondoni   au   Temeke. DHUMUNI   LA    MAFUNZO   HAYA  Dhumuni  kuu  la  mafunzo  haya  ni  kuwaandaa  wahitimu  kufanya  kazi  kama  WAALIMU  WA  UJASIRIAMALI  katika  Mradi  Wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini  unaoratibiwa  na  Taasisi.     MUDA  WA  MAFUNZO   Mafunzo   haya   yatafanyika   kwa   muda   wa   mwezi   mmoja   kuanzia   tareh

SULUHISHO LA CHANGAMOTO ZINAZO WAKABILI WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO TANZANIA

Mradi   wa   Elimu   Ya   Ujasiriamali   Mijini   na   Vijijini “ EUMIVI   PROJECT ” ni   mradi   unao   ratibiwa   na   Taasisi   ya   RafikiElimu   Foundation   kwa   kushirikiana   na   mashirika   rafiki.    Mradi   huu   ulizinduliwa   rasmi    tarehe   01   Septemba   2012   jijini   Dar   Es   salaam na   kuwahusisha   wajasiriamali   wadogo   wadogo   wa   jijini   Dar   Es   salaam   ambao   walipewa    mafunzo   ya   utengenezaji   wa   bidhaa   mbalimbali   kama   vile   sabuni   za   aina   zote, chaki   na   mishumaa   kwa   kutaja   vichache.   Baada   ya   hapo   mafunzo   yalielekea   katika   jiji   la   Arusha   ambapo   wajasiriamali   mbalimbali   wa   jijini   Arusha   walipatiwa   mafunzo   ya   utengenezaji   wa   bidhaa   mbalimbali. Mafunzo   haya   yalifanyika   pamoja utafiti   uliokuwa   ukifanywa   na   taasisi   hii   kuhusu   changamoto   mbalimbali   zinazo   wahusu wajasiriamali   wadogo   nchini   Tanzania. Utafiti   huo   wenye   kichwa   “ C