Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2013

HII NDIO KUMBUKUMBU YA MIAKA 17 YA AJARI YA MELI YA MV BUKOBA ILIYOZAMA TAREHE 21 MAY

Meli ikiwa inazama na ikiwa imezungukwa na mitumbwi pamoja na boti ambazo zilisaidia kwenye uhokoaji   MV Bukoba ikiwa inazama ilikuwa ni tarehe 21 mei 1996    Makaburi ya Igoma ambako ndugu zetu waliokuwa wakisafiri kwa meli ya MV Bukoba walizikwa. RIPOTI ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, iliyochunguza chanzo cha ajali ya mv Bukoba, inasema usiku wa kuamkia siku ya ajali, meli hiyo ilipakia abiria kati ya 750 na 800 pamoja na wafanyakazi 37. Kati ya hao, 114 waliokolewa wakiwa hai; wakati 391 waliopolewa wakiwa wamefariki na kuzikwa katika makaburi ya Igoma, nje kidogo ya Jiji la Mwanza. Miili mingine ilichukuliwa na jamaa kuzikwa kwao. Jumla ya miili 332 haikupatikana.   Kila mwaka, ifikapo Mei 21, serikali inayosema haina dini, huongozana na viongozi wa madhehebu ya dini na waganga, kwenda eneo la ajali kufanya kumbukumbu.   Serikali ilishitaki aliyekuwa nahodha wa mv Bukoba, Jumanne Rume-Mwiru, (sasa marehemu), Mkaguzi wa Mamlaka ya Bandari Gilbert Mokiwa; al

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MOROGORO.

                                NAFASI   ZA   MAFUNZO   YA   UJASIRIAMALI   MJINI  MOROGORO . RAFIKIeLIMU    MOROGORO    wanakuletea     SEMINA   YA   MAFUNZO   YA   UJASIRIAMALI . Mafunzo   yatakayo   fundishwa   ni   pamoja   na   Utengenezaji   wa   bidhaa   mbalimbali   kama   vile   ; Sabuni   za   aina   mbalimbali,   chaki, mishumaa, usindikaji,    utengenezaji   wa   manukato (   perfumes ), lotion, mafuta   ya   kujipaka, kiwi, mango   pickles, Chilly   Sauce, Tomato   Sauce    nakadhalika. WAPI  :  BERRICK EDUCATION CENTRE    karibu  na  SABASABA, mkabala na JENGO LA CCM MKOA MOROGORO.   . LINI    :   Tarehe    20    MEI   hadi   31  MEI   kuanzia   saa   nane  kamili  mchana  hadi  saa  kumi  na  mbili  jioni . ADA   YA   KUSHIRIKI   :   Shilingi    Elfu   Kumi  Tu  ( Tshs. 10, 000/=) Andika maombi yako kupitia barua pepe yetu : rafikielimutanzania@gmail.com 

UPDATE: WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MANZESE WAKUMBWA NA UGONJWA WA KUANGUKA

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Manzese iliyopo Manzese Uzuri, jijini Dar es Salaam wamevamiwa na mashetani na kuanguka hovyo darasani huku wakipiga kelele na kuongea maneno yasiyoeleweka na kusababisha hofu kutanda maeneo hayo. Tukio hilo limetokea kuanzia saa nne asubuhi ambapo alianza mwanafunzi mmoja kupiga kelele na kuanguka wakati wakiendelea na masomo ambapo alitolewa nje ya darasa lakini cha kushangaza waliendelea kuanguka wengine wengi huku wakipiga kelele na kupigana kama vichaa. PICHA  KWA  HISANI  YA  BLOGS  MBALIMBALI.

UFAFANUZI KUHUSU KUPITIWA UPYA KWA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012

UFAFANUZI KUHUSU KUPITIWA UPYA KWA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012 Mnamo tarehe 03 Mei, 2013 Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Wiliam Lukuvi (Mb) ilitoa Kauli ya Serikali Bungeni Kuhusu Taarifa ya Awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Sababu za kushuka kwa ufaulu wa Mtihani wa Kidato cha Nne Mwaka 2012. Kauli ya Serikali ilielekeza kuwa matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012 yafutwe na yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011 ili Wanafunzi hao wawe katika mazingira yanayofanana na ya wenzao wa miaka iliyopita kwa kuwa mfumo uliotumika mwaka 2012 katika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika mwaka 2011 na miaka iliyotangulia. Kwa kuzingatia mapendekezo ya Tume na Maelekezo ya Baraza la Mawaziri, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwar mamlaka aliyonayo chini ya Sheria ya Baraza la Mitihani Tanzania, kifungu cha 20, sura 107 ameliagiza Baraza la Mitihani la Taifa k

ALBINO AFUKUZWA SHULE JIJINI MBEYA KWA MADAI KWAMBA NI MCHAWI

Amina Mwamkinga alisema tangu tarehe tisa alipofukuzwa bwenini na wanafunzi wenzie wakitaka aondoke shuleni hapo wakimtuhumu kuwa mchawi majira ya usiku hali iliyomlazimu kuomba hifadhi kwa mlinzi aliyemkubalia na kukesha naye hadi asubuhi  hali iliyopelekea kupigwa na baridi kali kutokana na kukosa nguo za kujisitiri kama Shuka nk. Hapa Amina akimsimulia mkasa mzima mwandishi wa Mbeya yetu Joseph Mwaisango mara baada ya kupata maelezo yote ya Amina mwandishi wetu alimpigia simu katibu wa chama cha maalbino mkoa wa Mbeya afike ofisi ya Mbeya yetu ili wasaidiane kutatua tatizo hilo. katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale alifika ofisi ya Mbeya yetu na kuanza kumsikiliza Amina. katibu wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya, Wiliamu Simwale akiwa makini kumsikiliza Amina katika ofisi ya Mbeya yetu =========  ========  ============ KATIKA Hali isiyokuwa ya Kawaida Uongozi wa Shule ya Sekondari Hollwood iliyoko Mlowo Wilayani Mbozi Mkoa wa Mbeya

MWENYEKITI WA BARAZA LA MITIHANI - (NECTA ) ANADAI KUWA HAYUKO TAYARI KUYABADILI MATOKEO YA KIDATO CHA NNE -201

Kuna  tetesi  kwamba  Mwenyekiti wa Baraza la Mitihani la Taifa-NECTA ambaye pia ni Makamu Mkuuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Prof.Rwekaza Sympho Mukandala amegomai kubadili matokeo ya Kidato cha Nne- 2012. Chanzo cha karibu cha Prof.Mukandala kinadai kuwa mara baada ya kutolewa taarifa ya Serikali inayotaka 'kuboreshwa' kwa matokeo hayo,Prof.Mukandala ameonesha kukataa amri hiyo hadi sasa.  "Sisi tulipitisha matokeo hayo mbele yao na kwa idhini yao.Iweje leo Baraza libadili matokeo?.Tunafanya hivi kwa faida ya nani na kwa ustawi wa elimu ya wapi?" alinukuliwa akihoji Prof.Mukandala. Habari za kuaminka zinadai kuwa Prof.Mukandala pamoja na Katibu Mtendaji Dr.Joyce Ndalichako wanajiandaa kuachia ngazi kama Serikali itasimamia uamuzi wake huo.  Hata  hivyo, siku  za  hivi  karibuni  mwanahabari  wetu  alizungumza  na  Ofisa Habari wa NECTA, John Nchimbi ambaye alisema wamekwishapokea maelekezo kwa barua na kufanyia kazi ili kujitahidi ndani

NAFASI ZA MAFUNZO NA INTERNSHIP : MAY INTAKE

NAFASI ZA MAFUNZO NA INTERNSHIP : MAY INTAKE NAFASI   ZA   MAFUNZO   NA  INTERNSHIP Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation     inapenda  kuwatangazia  vijana  wa  kitanzania  nafasi  za  mafunzo : KOZI  ITAKA YO  FUNDISHWA :       HIV/AIDS  AND  COUNSELLING FOR  WOMEN. SIFA   ZA  MWOMBAJI  NAFASI : 1.Awe  wa  jinsia  ya kike ( Msichana/Mwanamke ) 2 Awe       mtanzania      mwenye    umri    wa    kuanzia    miaka    18  hadi    45. 3. Awe     na    elimu    ya    kuanzia  kidato  cha sita   nakuendelea au  awe  mwanafunzi  katika  taasisi yoyote   ya  elimu  ya  juu. 4. Anayeweza  kusoma  na  kuelewa  kwa  njia  ya  masafa  marefu.  6. Akiwa    na   ufahamu wa msingi   (   Basic   Knowledge   )   wa masuala   ya Research    atafikiriwa    kwanza. 7.  Awe  anaishi    katika  wilaya yoyote  iliyopo  Tanzania  bara. MUDA  WA  MAFUNZO   : Mafunzo  haya  yatafanyika  kwa  muda  wa  miezi  mitatu.  Mwezi  mmoja  utakuwa  ni  mafunzo  kwa  njia  ya  nadhar

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI ARUSHA.

                                NAFASI   ZA   MAFUNZO   YA   UJASIRIAMALI   JIJINI   ARUSHA. RAFIKIeLIMU     FOUNDATION    kwa   kushirikiana   na   Taasisi   ya     VISION   FOR   YOUTH   ya   Jijini   Arusha, wanakuletea     SEMINA   YA   MAFUNZO   YA   UJASIRIAMALI . Mafunzo   yatakayo   fundishwa   ni   pamoja   na   Utengenezaji   wa   bidhaa   mbalimbali   kama   vile   ; Sabuni   za   aina   mbalimbali,   chaki, mishumaa, usindikaji,    utengenezaji   wa   manukato (   perfumes ), lotion, mafuta   ya   kujipaka, kiwi, mango   pickles, Chilly   Sauce, Tomato   Sauce    nakadhalika. WAPI :    KWENYE   UKUMBI   WA   MAKUMBUSHO   ULIOPO   KARIBU   NA   MNARA   WA    MWENGE. LINI    :   Tarehe    20   hadi   21   Mwezi   wa   Tano   ( MEI )   kuanzia   saa   tatu   kamili   asubuhi   hadi   saa   tisa   kamili   alasiri. ADA   YA   KUSHIRIKI   :   Shilingi    Elfu   Ishirini   Na   Tano   Tu   ( Tshs. 25,000/=) Kwa   maelezo   zaidi   wasiliana   na   Uongo