Skip to main content

NAFASI ZA UFADHILI WA MASOMO YA SEKONDARI KWA YATIMA

RafikiElimu  FOUNDATION  ni  Taasisi  isiyokuwa  ya  kiserikali  inayo  jishughulisha  na  Maendeleo  ya  jamii. Taasisi  inapenda  kutangaza  nafasi  za  ufadhili  wa  masomo  ya  sekondari  kwa  waombaji  wenye  sifa  zifuatazo  :

1. Awe    yatima  wa  jinsia  ya  kike  au  awe  masichana  anayeishi  katika  mazingira  magumu.
2.Awe  raia  wa  Tanzania.
3. Awe  anajiandaa  kujiunga  na  masomo  ya  kidato  cha  kwanza  kuanzia  Januari  2013. AU
4. Awe  anajiandaa  kujiunga  na  masomo  ya  kidato  cha  tano   katika  mwaka  wa  masomo 2013/14.
5. Awe   ni  mwanafunzi  ambaye  tayari  anasoma sekondari   lakini   anashindwa/ ama  ameshindwa  kuendelea  na  masomo  yake  kutokana  na  kufiwa  na  wazazi ama  walezi wake.


*  N.B  : Ufadhili  wa  masomo  kwa  kidato  cha  tano  na  sita   utatolewa  kwa  wanao  taka  kuchukua  masomo  nya  michepuo  ya  ARTS.

Tuma  barua  yako  ya  maombi  ya  ufadhili  wa  masomo  kwenda  kwa :

MKURUGENZI  MTENDAJI,
RAFIKIELIMU   FOUNDATION,
S.L.P  35967,
DAR  ES  SALAAM.

*   Katika  barua  yako  ambatanisha  barua  ya  serikali  ya  mtaa  unaoishi, cheti  chako  cha  kuzaliwa ama  Hati  ya  Kiapo " AFFIDAVIT " , picha  zako nne  za  rangi, pamoja  na  vielelezo  vingine  vinavyo  thibitisha  kwamba  wewe  ni  yatima.

* Maombi  yako  yatufikie  kabla  ya  tarehe   07  JANUARY 2013.

*  Maombi  yanaweza  kutumwa  na  msimamizi  wa  mwanafunzi  husika  kwa  niaba  yake.

Comments

  1. asnte kwa huduma yenu nzuri nimeipenda,
    lakini naomba kufahamu jambo moja kuwa ni kwanini mnawasaidia jinsia ya kike tu ile hali kuna hata watoto wa jinsia ya kiume ambao hata wao pia ni yatima????
    wapo wengi wanatamani kupata msaada wa kimasomo je ni kwanini mko upande mmoja wa kike tu.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una