Skip to main content

SOMO LA TISA : USINDIKAJI WA MAZAO YA NAFAKA







Mahindi  yaliyo  toka  kuvunwa.




1.   USINDIKAJI  WA   ZAO  LA  MAHINDI :

Ili kuongeza matumizi ya mazao hayo na kudumisha ubora wake ni muhimu teknolojia za
kusindika nafaka zitumike. Usindikaji pia huongeza thamani ya zao.

                            KUSINDIKA MAHINDI

Punje za mahindi hutumika kupika makande na husindikwa kupata unga unaotumika katika
matumizi mbalimbali. Vile vile bidhaa nyingine zinazotokana na mahindi ni mafuta na wanga.

KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA

Kuna aina mbili za unga wa mahindi, unga wa mahindi yasiyokobolewa(Dona) na unga wa
mahindi yaliyokobolewa (Sembe)

 KUSINDIKA MAHINDI KUPATA UNGA WA DONA

Vifaa
• Mashine ya kukoboa
• Mashine ya kusaga
• Ungo
• Debe
• Mifuko
• Chekeche ya nafaka
Jinsi ya kusindika
• Pepeta na pembua mahindi ili kuondoa vumbi na takataka nyingine kwa kutumia chekeche,
ungo au sinia.
• Osha kwa maji safi na salama
• Anika kwenye chekeche safi ili yakauke
• Saga mahindi kupata unga


• Fungasha kwenye mifuko safi na kavu ya pamba, plastiki/nailoni, makaratasi yasiyopitisha
unyevu kisha hifadhi katika sehemu safi na kavu

Kumbuka: Kusaga mahindi bila kukoboa hudumisha virutubishi vilivyomo kwenye mahindi na
kupunguza upotevu wa chakula.

UNGA WA MAHINDI YALIYOKOBOLEWA

Jinsi ya kusindika
• Pepeta na pembua mahindi ili kuondoa vumbi na takataka nyingine kwa kutumia chekeche,
ungo au sinia
• Koboa na saga
• Fungasha kwenye mifuko safi na kavu ya pamba, plastiki/nailoni na ya karatasi isiyopitisha
unyevu.
• Hifadhi kwenye sehemu safi na kavu

Kumbuka:Kusaga mahindi yaliyokobolewa hupunguza virutubishi na wingi wa chakula kwa kiasi
cha asilimia 17 hadi 33.
Matumizi ya unga wa mahindi
Hutumika kutengeneza vyakula mbalimbali kama vile ugali, uji, togwa na vyakula vya watoto.
Pia huchanganywa na shayiri na kutengeneza vinywaji kama vile bia.




Mchele  baada  ya  kukobolewa.




2.  KUSINDIKA MPUNGA
Mpunga husindikwa kupata mchele ambao pia husindikwa kupata unga.
Kusindika mpunga kupata mchele
Vifaa
• Mashine ya kukoboa
• Madebe
• Ungo
• Chekeche
• Vifungashio

Jinsi ya kusindika
• Anika mpunga juani kwa muda wa siku moja kisha uache upoe kwa usiku mmoja ndipo
ukoboe.
• Pepeta na pembua kutoa takataka kabla ya kukoboa
• Koboa kwa kutumia mashine.

Kufungasha
Baada ya kupanga madaraja fungasha kwenye mifuko isiyopitisha unyevu na hifadhi katika
sehemu kavu na safi.

Matumizi ya mchele

Mchele hutumika kutengeneza vyakula mbalimbali kama vile wali, uji, biriani, mseto, pilau, bisi,
tambi na vitafunwa. Chenga za mchele hutmika kwa kutengeneza chakula cha mifugo.


KUSINDIKA MCHELE KUPATA UNGA
Vifaa
• Mashine ya kusaga
• Vifungashio

Jinsi ya kutengeneza
• Saga mchele safi kupata unga
• Fungasha kwenye mifuko safi na kavu isiyopitisha unyevu
• Hifadhi katika sehemu safi na kavu.
Matumizi ya unga wa mchele
Hutumika kupika ugali, uji na vitafunwa. Virutubishi vinavyopatikana kwenye unga wa mchele ni
kama vile vilivyoainishwa kwenye virutubishi vya mchele.


3.  KUSINDIKA MTA M A / UWELE
Punje za mtama na uwele hupikwa makande na husagwa kupata unga.
 KUSAGA MTAMA/ UWELE KUPATA UNGA:
Vifaa
• Mashine ya kusaga
• Ungo
• Chekeche ya nafaka
• Kichanja
• Turubai
• Vifungashio safi

 
Jinsi ya kusaga unga

• Pepeta na kupembua mtama/ uwele ili kuondoa mavumbi na takataka nyingine. Tumia
chekeche au ungo kupepeta na kupambeua
• Osha kwa maji safi kisha anika juani kwenye kichanja au turubai
• Saga kupata unga wa mtama/uwele
• Fungasha kwenye mifuko ya nailoni/ plastiki
• Hifadhi katika sehemu safi na kavu
Matumizi ya unga wa mtama/ uwele
Hupikwa ugali, uji na togwa. Vile vile htumika katika kutengeneza vyakula vya watoto






Ngano.

4.  KUSINDIKA NGANO

Ngano husagwa ili kupata unga
Vifaa
• Vifungashio
• Mashine ya kusaga
Jinsi ya kusaga
• Nyunyuzia maji kwenye ngano
• Koboa na saga ili kupata unga
• W eka kwenye vifungashio safi na visivyopitisha maji
Matumizi
• Unga wa ngano hutengeneza vitafunwa kama vile mikate, chapati, maandazi, tambi na
keki.
• Hutumika katika mapishi mbalimbali

SOMO  LA  KESHO :  USINDIKAJI  WA  MAZAO  YA  MIZIZI.

Comments

  1. Masomo mazuri sana nime elimika.bado nataka kujua ukitaka kuhifadhi mahindi kwa mwaka mmoja bila kuharibika,mpunga na nafaka nyingine

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una