Skip to main content

SOMO LA TANO : UTENGENEZAJI WA TOMATO SOUCE.

Maandalizi  ya  utengenezaji  wa  Tomato  Souce.


Tomato  Souce.

MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KWENYE  UTENGENEZAJI  WA  TOMATO  SOUCE.

1. Nyanya            Kg  1.5 (  Kilo  moja  na  nusu  )
2.Vitunguu  Maji.      Vitatu  vilivyo  menywa  na  kukatwa  katwa  vipande.
3. Mafuta  ya  Kupikia     Vijiko  Sita  Vya  Chakula.
4. Sukari                        Vijiko  viwili  vya  chai.
5. Citric  Acid.
6.Vinegar.                          Vijiko  viwili  vya  chai.

HATUA  ZA  KUFUATA  WAKATI  WA  UTENGENEZAJI  WA  TOMATO  SOUCE. 


Tomato  Souce  iliyo  katika  hatua  za  maandalizi 



1. Saga  mchanganyiko  wa  malighafi  zote  zilizo  tajwa  hapo  juu  kwa  pamoja  kwa  kutumia  mashine  ya  blender  mpaka  uwe  rojo  rojo.

2. Tenga  jiko  la  mkaa  lenye  moto  wa  wastani, kisha  injika kikaangio  kwenye  moto  halafu  weka  mafuta  ya  kupikia  vijiko  sita   vya  chakula.
3. Mafuta  yakianza  kuchemka , anza  kumimina  mchanganyiko  wako  huo  ndani  ya  kikaango  hicho   huku  ukiwa  una  koroga  upande  mmoja  mpaka  umalize  kuchanganya. Tumia  dakika  15  kufanya  zoezi  hili.

*  Utakapo  ona  mchemsho  wako  umeanza  kuwa  uji  uji, ipua  na  weka kwenye  chombo  safi  tayari  kwa  matumizi.

Comments

  1. Citric Acid inatakiwa kiasi gani ili kuweka uwiano ulio sahihi bila kuasili afya za watumiaji?

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una