Skip to main content

SOMO LA SABA : UTENGENEZAJI WA WINE YA NDIZI

Wine  ya  Ndizi.
 Wine  ya  ndizi  inatokana  na  ndizi  mbivu.  Aina  yoyote  ya  ndizi  ambayo  inaweza  kuwiva  inaweza  kutumika  kutengeneza  wine.

Ili  wine  yako  iweze  kuwa  na  kilevi  ni  lazima  uichanganye  na  amira, usipoweka  amira  wine  yako  itakuwa  tamu  lakini  isiyokuwa  na  kilevi.

MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NDIZI.

*  Ndizi   zilizo  iva  vizuri.

* Maji

*  Vyombo  vya  kuhifadhia.

*  Amira

* Sukari.


HATUA  ZA  KUFUATA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NDIZI.

                                              HATUA  YA  KWANZA :

*  Chukua   ndizi  kg.3  zilizo  menywa  maganda  na  ambazo  zimeiva  vizuri, katakata   vipande  vidogo  na  weka  katika  chombo  ambacho  utatumia  kuchachulia  wine  yako.


*  Baada  ya  kupata  hivyo  vipande  vidogo  vidogo , vichanganye  kwenye  maji  lita  ( 5 )  na   baada  ya  hapo  chemsha   kwa  muda  wa  dakika  30.

* Acha  mchanganyiko  wako  huo  upoe.

                                                    HATUA   YA  PILI

*  Changanya  mchanganyiko  wa  ndizi  na  sukari  kikombe  kimoja   cha  chai, koroga  kisha  changanya  na  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  sukari, koroga  tena.

*  Acha  kwa  muda  wa  siku  nne,   siku  ya  nne  utakapo  kwenda  kuitazama  wine  yako  utakuta  povu, hii  ina  maana  kuwa  wine  yako  itakuwa  imeanza  kuchachuka   vizuri.

*  Siku  ya  tano  (  5  )  chuja  wine  yako  vizuri  kwa  kutumia  kitambaa  lakini  bila  kufinyanga, iache  wine  imwagike  yenyewe.

                                               HATUA  YA  TATU 

* Iweke   wine  yako  kwenye  chombo  cha  kutolea  hewa  na   kupunguza  gas  kwa  siku  1  mpaka  miezi  3.

*  Baada  ya  siku  21  wine  yako  itakuwa  tayari.

Comments

  1. kwenye picha mnatuonyesha ndizi lilizokatwakatwa na maganda lakini kwenye maelezo mnasema zilizo menywa! hii inamaanisha kuficha utaalamu au kujisahau?

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una