Skip to main content

SOMO LA PILI : UTENGENEZAJI WA MISHUMAA.


Mishumaa., Utengenezaji  wa  mishumaa  huweza  kusaidia  kuongeza  kipato  cha  mjasiriamali, kwani  bidhaa  hii  huitajika  sana  kwa  matumizi  mbalimbali  kama  vile  matumizi  ya  majumbani  nakadhalika.
 MALIGHAFI   ZINAZO  HITAJIKA  WAKATI  WA  UTENGENEZAJI  WA  MISHUMAA.

1. Paraffin  Wax
2. Utambi
3. Mould  (  Umbo )
4.  Stearine  au  mixture
5. Rangi
6. Jiko  la  mafuta  ya  taa  au  mkaa.
7. Sufuria.
8. Boric  acid.



Paraffin  Wax. 





:
VIDOKEZO  MUHIMU :
1. Paraffin Wax :
Hii  inatokana  na  nta  na  sega  ya  nyuki   iliyo  changanywa  na  mafuta  ya  taa.  Ina  rangi  nyeupe  na  katika  utengenezaji  wa  mishumaa  ina  ubora  kuliko  bee  wax.

     *  Bee  Wax   :  Inatokana   na  masega  ya  nyuki   yaliyo  changanywa  na  mafuta  ya  petroli  na  diesel  na  rangi  yake  ni  ya  njano.

2. STEARINE 
Hii  dawa  maalumu  inayo  fanya  mishumaa  iungane  ama  ishikamane.

Mould ( Umbo )  . Mfano  wa  umbo  linalo  weza  kutumika  kutengeneza  mishumaa. Hata  hivyo, unaweza  kutengeneza  umbo  lolote  kwa  kadri  unavyo  taka  " shape "  ya  mishumaa  yako  iwe. 
3. BORIC  ACID  :  Hii  ni  maalumu  kwa  ajili  ya  kuufanya  utambi  usiishe  mapema  na  uwake  bila  kutoa  moshi.

4. RANGI  :  Rangi  nzuri  zinazo  tumika  katika  utengenezaji  mishumaa  ni  rangi  za  chakula  na  nyingi  huwa   ni  za  maji.




Boric  acid  , hii  ni  maalumu  kwa  ajili  ya  kuufanya  utambi  usiishe  mapema  na  kuufanya  uwake  bila  kutoa  moshi.


                              JINSI  YA  KUTENGENEZA

Andaa  mould  (  umbo  lako  )  utakalo  litumia  baada  ya  kuyeyusha  (  paraffin  wax  )  na  kuchanganya  na  michanganyo  yote.

Kwa  Mfano :  (  Kipimo  cha  stearine  )
1. Wax  kilo  moja  -  Stearine  vijiko  vinne  vya  chakula.
2. Wax  nusu  kilo  -  Stearine  vijiko  vinne  vya  chakula
3. Wax  robo  kilo - Stearine  kijiko  cha  chakula.


*  Baada  ya  mould  (  umbo )  kuwa  tayari , chemsha  wax mpaka  iyeyuke  na  itoe  kwenye  vyombo  ambavyo  umetayarisha  na  usubiri  ikauke  ili  uanze  kutoa  mishumaa.

Comments

  1. post nzuri,ila wekeni vizuri zaidi. Mafano;boric acid hamjaweka vipimo vyake.
    Nadhani mgeweka step kwa step vipimo na michanganyo yake.

    Good job.

    ReplyDelete
  2. Umetueleza vizuri lkn kwa juu juu tu

    ReplyDelete
  3. Umetueleza vizuri lkn kwa juu juu tu

    ReplyDelete
  4. Naweza pata wapi hiyo wax kwa dar?

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una