Skip to main content

MASOMO YA UTENGENEZAJI WA BIDHAA MBALIMBALI KWA NJIA YA NADHARIA SASA KUPATIKANA MTANDAONI.

UONGOZI  wa  Taasisi  Ya  RAFIKIELIMU  FOUNDATION  unapenda  kuwafahamisha  wanafunzi  wote  walio  jiandikisha  katika  mafunzo  ya  ujasiriamali  yanayo  tolewa  na  taasisi  yetu  kupitia  Mradi  wa  Elimu   Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini " EUMIVI  Project "  kwamba  kuanzia  leo  tarehe  12  NOVEMBA  2012,  masomo  ya  UZALISHAJI &  UTENGENEZAJI  wa  bidhaa  mbalimbali  kwa  njia  ya  NADHARIA    yatakuwa  yakitolewa    online  kupitia  katika   blogu  yetu  hii.  Uamuzi  huu  umetokana  na  maombi  ya  watu  wengi . Utaratibu  utakuwa  kama  ifuatavyo; kila  siku  tutakuwa  tunatoa    somo  moja  au  masomo  mawili  au  zaidi, kulingana  na  nafasi  yetu    pamoja  na  ukubwa  wa  somo  husika. Jukumu  lako  litakuwa  ni kuyafuatilia  masomo  hayo  na  kuyafanyia  kazi.  

UTARATIBU  WA  MAFUNZO  KWA  NJIA  YA  VITENDO :
Kama  tulivyo  toa  maelezo  yetu  katika  semina  zetu  mbalimbali,  mafunzo  kwa  vitendo  yatakuwa  yakifanywa  kwa  makundi  ya  mawili  mawili, kila  kundi  likiwa  na   watu  ishirini.

Jukumu  lako  wewe  kama  mwanafunzi, wa  EUMIVI  ni  kutafuta  watu  kwa   ajili  ya kuunda  makundi  ya  kufanya  mafunzo  kwa  vitendo. Hii  ina  maana  kuwa  kila  mwanafunzi  wa  EUMIVI  anatakiwa  kuwa  kiongozi  wa  kundi  ama  makundi  ya  watu  atakao  waandikisha  katika  mradi. Isisahaulike  kuwa, malipo  ya  "  commission "  ya  shilingi  elfu  moja  kwa  kila  mtu  utakaye  muandikisha  katika  mradi  yapo  pale  pale.

KUMBUKA :  JUHUDI  zako  wewe  kama  mwanafunzi  wa  EUMIVI  , ndio  zitakazo  kufanya  upate  nafasi  ya  kuhudhuria  mafunzo  kwa  vitendo. Endapo  utashindwa  kutengeneza  kundi  la  angalau  watu  ishirini   au  zaidi  kwa  ajili  ya  kuhudhuria  mafunzo  kwa  vitendo, basi  amini  nakwambia  hutoweza  kupata  nafasi  ya  kuhudhuria  hayo  mafunzo    ya  vitendo  yanayo  tolewa  bure  kabisa  na  taasisi  yetu  kupitia  mradi  huu.

UNACHO  TAKIWA  KUFANYA  :  Unacho  takiwa  kufanya  ni  kuwaandikisha  watu  angalau  ishirini , na  kutuma  majina  yao  kwetu  kwa  njia  ya  barua  pepe, then  sisi  tutakutafutieni  tarehe  kwa  ajili  ya  kufanya  hayo  mafunzo  ya     vitendo.

TUNAOMBA  USHIRIKIANO  KUTOKA  KWENU.
ASANTENI.



Comments

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una