Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2012

ABG NORTH MARA YAGAWA MADAWATI 1,000 KWA SHULE ZA TARIME.

  Pichani Juu na Chini ni Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi zilizopo wilayani Tarime mkoa wa Mara wakifurahia msaada wa madawati zaidi ya 1,000 kutoka mgodi wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya African Barrick Gold (ABG). Wanafunzi wa shule za msingi za serikali za wilaya ya Tarime, mkoa wa Mara, wakikaa sakafuni kabla ya kupata msaada wa madawati zaidi ya elfu moja kutoka mgodi wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya African Barrick Gold (ABG). Msaada wa pikipiki tatu maarufu kama Bajaj ambazo mgodi wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya African Barrick Gold (ABG) ulitoa kwa baadhi ya wananchi wa jamii zinazoishi karibu na mgodi huo uliopo wilaya ya Tarime mkoa wa Mara. TARIME Mgodi wa dhahabu wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya African Barrick Gold (ABG) umetoa msaada wa madawati zaidi ya 1,000 kwa shule za msingi zilizopo wilayani Tarime, mkoa wa Mara. Msaada huo utakaoenda k

MRADI WA " ELIMU YA UJASIRIAMALI MIJINI NA VIJIJINI" WAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

Mwalimu  wa  Ujasiriamali  kutoka  katika  Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, Mama  Ashankira  Lupembe  , akifundisha  kwa  vitendo  namna  ya  kutengeneza  sabuni   ya  maji. Mwanafunzi  wa  ujasiriamali  akitengeneza  sabuni  ya  unga  mwenyewe  mara  baada  ya  kupata  maelekezo  kutoka  kwa   waalimu  wa  ujasiriamali  kutoka  RafikiELIMU  Foundation. Mwanafunzi  wa  ujasiriamali  akitengeneza  sabuni  ya  maji  kwa  vitendo   mara  baada  ya  kupata  maelekezo  kutoka  kwa   waalimu  wa  Ujasiriamali  kutoka  katika  Asasi  ya  RafikiElimu  Foundation. Wajasiriamali  wakifanya  "  practical "  ya  kutengeneza  sabuni  ya  maji  kwa  vitendo  mara  baada  ya  kupokea  maelekezo  kutoka  kwa  waalimu  wa  ujasiriamali  kutoka  katika  Asasi  ya  RafikiElimu   Foundation.  Mwalimu  wa  Ujasiriamali  kutoka  Taasisi  ya  RafikiElimu   Foundation, Mama  Hellen  Mbise  akielekeza  kwa  vitendo  namna  ya  kutengeneza  sabuni   za  maji.  Mwalimu  Ashankir