Skip to main content

Rafiki Elimu Foundation Yawalipia Ada Yatima Mia Moja Kumi na Tano wa Kike shule za skondari Vijijini.

Katibu  Mkuu  wa  Taasisi  ya  Rafiki  Elimu  Foundation, Bwana  Omary  Baraka  Mbwetom (  wa  mwisho  waliosimama )  akiwa  katika  picha  ya  pamoja na  baadhi  ya  wanafunzi   na mwalimu wa    Shule  Ya  Sekondari  Ya   Kisaza  iliyopo  Wilayani  Handeni  Mkoani  Tanga.
Wanafunzi  wa  Shule  ya  Sekondari  Pangambili  iliyopo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga  wakilima.
Wanafunzi  wa  Shule  ya  Sekondari  Pangambili  iliyopo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga. 
Wanafunzi  wa  Shule  ya  Kwaludege  Sekondari  wakichota  maji  bwawani  kwa ajili  ya  matumizi mbalimbali.
Wanafunzi  wa  Shule  Ya  Sekondari  Kisaza, iliyipo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga.
Kabuku  Secondary  School, Handeni, Tanga.
Wanafunzi  wa  Kabuku  Sekondari  School, iliyipo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga.
Shule  ya Sekondari  Kwaludege  iliyopo  wilayani  Korogwe, mkoani  Tanga.
Wanafunzi  wa  Shule  ya Sekondari  Kwaludege  wakiwa  katika  picha  ya  pamoja  na  Katibu  Mkuu  wa  Rafiki  Elimu  Foundation  pamoja  na  walimu  wa  shule  hiyo.
Wanafunzi    yatima  wa  kike  na  wanaoishi  katika  mazingira   magumu  wapatao  mia  moja  kumi  na  watano (  115 )  wanao soma    katika  shule  za  sekondari  za   Kwaludege  Secondary  School,   Pangambili  Secondary  School,  Kabuku  Secondary  School   pamoja  na  Kisaza  Secondary  School  zilizopo  katika  wilaya  za  Handeni  na  Korogwe Mkoani  Tanga. wamefanikiwa  kupata  udhamini  wa  kusomeshwa   kwa  kulipiwa ada  ya  shule  pamoja  na   vifaa  vinginevyo  muhimu  katika  masomo kama  vile  vitabu  vya ziada  na  kiada.
Udhamini huo, umetolewa  na  Asasi  Isiyokuwa  ya  Kiserikali  iitwayo  "  Rafiki  Elimu  Foundation " ya jijini  Da  Es  salaam  kupitia  mradi  wake  "  Elimisha  Msichana  Project "  uliolenga  katika  kutoa  msaada  wa  kuwasomesha  wanafunzi  wa  kike  wanao  soma  katika  shule  za  sekondari  zilizopo maeneo  ya vijijini  na  ambao wanaishi  katika  mazingira  magumu( mfano  watoto  yatima, na  wale  wenye wazazi  wazee  ama  walemavu ) kwa  kuwalipia  ada  pamoja  na  kuwapatia vifaa vingine  muhimu  katika  masomo  kama  vile  vitabu  vya  ziada  na  kiada. Walengwa  wakuu  katika  mradi   huu  ni  wanafunzi  wa  kike  katika  shule  za  sekondari  zilizopo  maeneo  ya  vijijini  na  ambao wanaishi  katika  mazingira  magumu, mfano yatima, wenye  wazazi  wazee  sana  na  walemavu.

Akiongea  na   waandishi  mbalimbali  wa  habari, Katibu  Mkuu  wa  Taasisi  ya  Rafiki  Elimu  Foundation,  Bwana, Omary  Baraka  Mbweto, amesema  yakuwa , lengo  la  mradi  ni  kuhakikisha  wanawasaidia  wasichana  elfu  tano  wanaosoma  katika  shule  za  sekondari  zilizopo  vijini    na  wanaoishi  katika  mazingira  magumu  katika   mikoa  yote  ya Tanzania  Bara, ambapo  kwa  kuanza    taasisi  yake  imeanza  na  kuwalipia  ada  za  masomo  pamoja  na  vifaa  mbalimbali  vya  shule  wanafunzi  wapatao  mia  moja  na  kumi na  tano  katika  wilaya  ya  Handeni  ambayo  ipo  katika  mkoa  wa   Tanga.

Katibu  Mkuu  wa  Rafiki  Elimu  Foundation (  Wa  Pili  kutoka  kulia, waliosimama  ) akiwa na  wanafunzi  wa  Shule  ya  Sekondari  Kwaludege, iliyopo  Handeni, Mkoani  Tanga  ambao  wanafadhiliwa  na  Taasisi  ya  Rafiki  Elimu  Foundation. Wa  kwanza kulia ( waliosimama/aliye  vaa  shati  la  buluu ) ni  Mwalimu  katika  shule  hiyo  ya  sekondari.
" Mradi  huu, hautaishia hapahapa   Handeni, Tanga  bali  utakuwa  ni  mradi   wa  nchi  nzima, baada  ya  hapa  tutaelekea  wilayani Manyara  ambapo  tunaenda  kufanya  utafiti   katika  wilaya  ya  Babati  na kutoa  msaada  wetu huo,  kabla  ya  kuelekea  katika  wilaya  za  Kondoa  ( Dodoma )    Arumeru (  Arusha  ).  Mkuranga, Rufiji, Kisarawe  na  Mafia (  Pwani ).  Alisema   Ndugu  Mbweto.   " Tukimalizana  na  wilaya  hizo  tutaelekea katika wilaya  nyinginezo  za  Tanzania  Bara " aliongeza.

Bwana  Omary  Mbweto  alisema  kuwa,  ili  kuhakikisha  kuwa  wanafunzi  wanao saidiwa  katika  mradi huu ni  wale wenye  uhitaji  kweli, yani yatima,  watoto wenye  wazazi  wazee  sana  ama  walemavu, taasisi  yake  imekuwa  makini  mno  kwa  kuhakikisha  kuwa   nyaraka zote  muhimu  zinazo  thibitisha  kuwa  mwanafunzi  husika    ni  yatima   na  ama  ana  ishi  katika  mazingira  magumu.

Mradi  wa  Elimisha  Msichana  Project  mbali  na  kuwalipia  ada  na   mahitaji  muhimu  ya  shuleni  kama  vile vitabu  na   kiada  na  ziada  wanafunzi wa kike  yatima  wanaoishi  katika mazingira  magumu  waliopo  katika  shule  za  sekondari  zilizopo  katika  maeneo  ya  vijijini  nchini  Tanzania, pia  umelenga  kutoa  elimu  kwa watanzania  wote  kuwahasisha  kujenga  utamaduni wa  kuwasomesha  watoto wa  kike, na  yatima  wanaoishi  katika  mazingira  magumu.

Mbali  na  kujihusisha  na  maendeleo  ya  elimu  nchini  Tanzania,  taasisi ya  Rafiki  Elimu Foundation   inahusika  na  kutoa  msaada  wa  kisheria  kwa   watu mbalimbali  wenye  matatizo  ya  kisheria  lakini  hawana  uwezo  wa  kumudu  gharama  za  mawakili, huku  kipaumbele kikiwekwa  zaidi  kwa  wanawake, walemavu, wazee  na  katika masuala  ya  elimu.

Comments

  1. To me i would like to join this RafikiElimu Foundation programs but i search for the table of registration process in mwanza but there is a list of starting class period in mwanza and morogoro.So please i would like to know the time of registration in mwanza for those not yet registed.Because i am the among not yet registed but i would like to be among the students in that program.And me I'm from mwanza -Tanzania.

    ReplyDelete
  2. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  3. habari naitwa simon dominick, natafuta mfadhili wa kunisomesha kwa sasa nasoma chuo cha biashara cbe, wazazi wangu hawana uwezo wa kunisomesha, kama kuna msamaria mwema naomba anisaidie

    0717697657
    simondominick@yahoo.com

    ReplyDelete
  4. Grace Nursery school seeks your support in establish a better system for learning and to help raise young leaders of tomorrow to realise their future dream and grow spiritually.
    The school is based in Mbeya Tanzania and it's under only 3 teachers,your support is really needed in improving the istitution.
    your support in any way will be greatly appreciated.
    for more information:
    Phone number:+254721452113
    +255754749035
    Email address:hb2samweli@yahoo.com
    hb2samweli@gmail.com
    Fb account:Grace nursery & primary school

    ReplyDelete
  5. your support is very important, keep supporting these vulnerable ones

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SOMO LA TATU : UTENGENEZAJI WA UNGA LISHE.

Mahindi   ni  miongoni  mwa  mazao ya  chakula  ambayo  unga  wake  unatumika  kutengeneza    unga  lishe. UNGA  LISHE  :  Ni  unga  bora  na  unao  hitajika  sana  katika  kuborehs  afya  za  watoto, wazee  na  wagonjwa.  Ukiwa  kama  mjasiriamali  mdogo, ni  muhimu  kujua  namna  ya  kutengeneza  unga  lishe, kwani  malighafi  zinazo  tumika  katika  utayarishaji  wa  unga  huu  zinapatikana  kwa  wingi  na  kwa  bei  nafuu, hivyo  basi  hata  kwa  wewe  mwenye  mtaji  mdogo,  unaweza   kufanya  biashara  hii   bila  ya  kuhitajika  kuwa  na  mtaji  mkubwa  jambo  linalo  chukuliwa  kama  changamoto  kwa  wajasiriamali wengi  nchini. MCHELE. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  UNGA  LISHE. * Karanga    - Nusu  Kilo. * Soya         - Nusu  Kilo. * Ulezi         -   Kilo  moja  na  Nusu. * Mahindi    -Nusu  Kilo *Mtama     - Mtama  Nusu  Kilo. * Uwele     -  Nusu  kilo. * Mchele    -  Nusu  kilo.. JINSI  YA  KUTENGENEZA  UNGA  LISHE . 1. S

NAFASI ZA KUJITOLEA SINGIDA

Taasisi  ya  ORPHANS  &  VULNARABLE   CHILDREN  CARE    (  OVCC  )  ya  Mjini  SINDIDA  inatangaza  nafasi  za  kazi  za  kujitolea  kama  ifuatavyo  : Picha  za  matukio  ya  shughuli  mbalimbali  za  Taasisi  ya OVCC.   1.       Miandi Secondary school:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-          (i) Physics               2          (ii) Chemistry           2          (iii) Biology              2          (iv) Geography         1          (v) Basic Mathematics. 2 2.         Puma Secondary School:-       Volunteers wa masomo yafuatayo:-         (i) Fnglish                        2         (ii) Physics                      3         (iii) Chemistry                  3                        (iv) Biology                      3         (v) Basic Mathematics     4 3.       Puma Dispensary:-     Volunteers wa Taaluma zifuatazo:-       (i) Taaluma ya Utabibu             8       (ii) Taaluma ya Kinga ya Afya   8

SOMO LA NANE : KUTENGENEZA WINE YA NANASI.

Nanasi.  Wine  ya  nanasi  ni  rahisi  kutengeneza  kwa  sababu  mananasi  yanapatikana  kwa  wingi  sana  katika  kipindi  kirefu  cha  mwaka. MALIGHAFI  ZINAZO  HITAJIKA  KATIKA  UTENGENEZAJI  WA  WINE  YA  NANASI. * Nanasi. *  Maji. * Sukari. * Amira. HATUA  YA  KWANZA  KUTENGENEZA *  Menye  maganda  ya  mananase  na  kupata  nyama . ( Kinacho  tumika  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenyewe  na  sio  maganda  ya  mananasi  ) *  Katakata  vipande  vidogo  kisha  weka  katika  chombo  kwa  ajili  ya  kuchemsha,  nanasi  linalo  faa  katika  utengenezaji  wa  wine  ya  nanasi  ni  nanasi  lenye  uzito  wa  kg. 5. * Chemsha  kwa  muda  wa  dakika  30  kwa  moto  wa  kawaida (  Inashauriwa  kutumia  moto  wa  mkaa  ) * Baada  ya  kupoa   anza kuchachua  kwa  kuweka  amira   vijiko  vinne (  4  )  vya  chakula ,  sukari  vijiko  viwili  vya  chai na  kisha  koroga  kwa  muda  wa  dakika  20. *  Acha  kwa  muda  wa  dakika  5  ukiwa  una