Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2012

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

RafikiElimu   Foundation     wanatangaza  nafasi za  mafunzo  ya  ujasiriamali .  Mafunzo  yatakayo  tolewa  ni  pamoja  na  : 1.   Kutengeneza  sabuni 2.  Kutengeneza    chaki 3.Kutengeneza  mishumaa. 4.Kutengeneza   viatu  vya  ngozi. 5. Kutengeneza  mkaa  kwa  makaratasi. 6. Kutengeneza  batiki. 7. Uokaji  mikate 8. Usindikaji  wa   vyakula  na  vinywaji  pamoja  na 9.  Uongozi  wa   biashara. WALENGWA   WAKUU  WA  MAFUNZO /  SIFA  ZA   WASHIRIKI Ili  uweze  kupata   nafasi  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  unatakiwa  uwe  na  sifa  zifuatazo: 1.  Uwe  raia  wa  Tanzania. 2. Uwe  na  umri  wa  kuanzia  miaka  16  na kuendelea. 3. Uwe  unajua  kusoma  na  kuandika . ADA  YA  KUSHIRIKI  KATIKA  MAFUNZO Ada  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  ni  shilingi   Elfu  Ishirini  na  Tano  Tu (  Tshs.  25,000/=) MALIPO  YA  ADA Malipo  ya  ada  ya  mafunzo  yafanyike  kupitia   CRDB  BANK ,  Account  number 0152395997900 ,   Jina  la  Akaunti  ni     RAFIKI  EL

KUTOKA TUNDUMA : MAANDAMANO YA WANAFUNZI YASABABISHA VURUGU, POLISI WALAZIMIKA KUTUMIA MABOMU YA MACHOZI..

Wanafunzi na wananchi wakiwa wanachoma baadhi ya Maeneo Tunduma   Wananchi wa Tunduma wakiwa wanashuhudia Live tukio la wanafunzi wa shule za Msingi Tunduma walipo goma  Njia ya Kuelekea Boda la Tunduma ikiwa imefungwa Wananchi wa Tunduma wakiwa wanashuhudia Live tukio la wanafunzi wa shule za Msingi Tunduma walipo goma      KUTOKA  WILAYANI  TUNDUMA  :  Maandamo  ya  wanafunzi  yasababisha  vurugu , polisi  walazimika  kutumia    mabomu  ya  machozi  kutawanya  maandamo  ya  wanafunzi. PICHA  NA  HABARI  ZOTE  NI  KWA  MUJIBU  WA  ;  WWW.MBEYAYETU.BLOGSPOT.COM . Kutoka  RafikiElimu :  Tunaiomba  serikali  imalize  mgogoro  huu  haraka  iwezekanavyo  ili  wanafunzi  warudi  darasani  na  kuendelea  na  masomo  yao  kama  kawaida. Mungu  Ibariki  Tanzania, Mungu  Ibariki  Afrika.

KUTOKA SHULE YA MSINGI VWAWA ILIYOPO MANISPAA YA MBEYA, WANAFUNZI WAANDAMANA HADI KWA MKUU WA WILAYA

Wanafunzi wa shule za msingi Vwawa wakiwa wanapiga vidumu huku wakielekea ofisi ya mkuu wa wilaya ni Baada ya walimu kugoma. Wanafunzi  wa  Shule  ya  msingi  Vwawa  iliyopo  katika  manispaa  ya  Mbeya  wakiandamana  kuelekea  katika  ofisi  ya  Mkuu  wa  Wilaya   ya  Mbeya   . Kufuatia  mgomo  wa  walimu  ulioandaliwa  na  Chama  Cha  Waalimu  Tanzania, " CWT "   kuanzia  tarehe  30 Julai  2012    kwa  muda  usiojulikana  hadi  hapo  serikali  itakapo   timiza  madai  yao, wanafunzi  wa  Shule  Ya  Msingi  Vwawa  iliyopo  katika  manispaa   ya  Mbeya, waamua  kuandamana   hadi  katika  ofisi  ya  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Mbeya,  kuishinikiza  serikali   kuwatimizia  walimu  madai  yao  ili  waweze  kuendelea   na  masomo  yao.  Picha  na  habari   kutoka   :  www.mbeyayetu.blogspot.com

KILICHOJIRI KWENYE MGOMO WA WALIMU MKOANI MBEYA

Mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi muungano akiwa nje ya shule akichezea mchanga maana walimu wamegoma   Wanafuzi wapo makini kumsikiliza mwanafunzi mwenzao Wanafanzi wa darasa la saba shule ya msingi Meta wakiendelea kupeana mazoezi ya masomo mbalimbali baada ya waalimu wao kugoma kuingia madarasani  Shule ya msingi Meta

MGOMO WA WAALIMU UNAVYO WAATHIRI WANAFUNZI

Juu  wanafunzi  wa  shule  za  msingi   Ipembe, Nyerere, na  Unyankindi  zilizopo  katika  manispaa  ya  Singida  wakiwa  katika  maandamano.   Mwanafunzi  akiwa  anawafndisha  wanafunzi  wenzake  baada  ya  walimu  kugoma. Hii  imetokea  huko  mkoani  Mbeya  siku  ya   jana  tarehe  30  Julai  2012. Picha  kwa  hisani  ya  MJENGWA  BLOG .  Mgomo  uiso  na  kikomo  ulio  andaliwa  na  Chama  Cha  Waalimu  Tanzania   ( CWT )  ambao  umeanza  rasmi  siku  ya    tarehe  30  Julai  2012   kwa  muda  usiojulikana  hadi  hapo  serikali  itakapo  sikiliza  matakwa  ya  waalimu, umekuwa  na  athari  kubwa  sana  kwa  wanafunzi. Waathirika  wakuu  wa  mgomo  huu  ni  wanafunzi  ambao  wanajiandaa  na  mitihani  ya  taifa  ambayo  inakaribia   kuanza  kufanyika  nchi nzima , mfano  darasa  la  saba  nakadhalika. Sisi  kama  RafikiElimu   Foundation  tunaiomba    serikali   imalize  mgogoro  huu  haraka  iwezekanavyo   ili  watoto  wetu   waweze  kuendelea  na  masomo  yao  kama  kawaida.

NAFASI ZA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

RafikiElimu   Foundation     wanatangaza  nafasi za  mafunzo  ya  ujasiriamali .  Mafunzo  yatakayo  tolewa  ni  pamoja  na  : 1.   Kutengeneza  sabuni 2.  Kutengeneza    chaki 3.Kutengeneza  mishumaa. 4.Kutengeneza   viatu  vya  ngozi. 5. Kutengeneza  mkaa  kwa  makaratasi. 6. Kutengeneza  batiki. 7. Uokaji  mikate 8. Usindikaji  wa   vyakula  na  vinywaji  pamoja  na 9.  Uongozi  wa   biashara. WALENGWA   WAKUU  WA  MAFUNZO /  SIFA  ZA   WASHIRIKI Ili  uweze  kupata   nafasi  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  unatakiwa  uwe  na  sifa  zifuatazo: 1.  Uwe  raia  wa  Tanzania. 2. Uwe  na  umri  wa  kuanzia  miaka  16  na kuendelea 3. Uwe  unajua  kusoma  na  kuandika . ADA  YA  KUSHIRIKI  KATIKA  MAFUNZO Ada  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya  ni  shilingi   Elfu  Ishirini  na  Tano  Tu (  Tshs.  25,000/=) MALIPO  YA  ADA Malipo  ya  ada  ya  mafunzo  yafanyike  kupitia   CRDB  BANK ,  Account  number 0152395997900 ,   Jina  la  Akaunti  ni     RAFIKI  ELI

Rafiki Elimu Foundation Yawalipia Ada Yatima Mia Moja Kumi na Tano wa Kike shule za skondari Vijijini.

Katibu  Mkuu  wa  Taasisi  ya  Rafiki  Elimu  Foundation, Bwana  Omary  Baraka  Mbwetom (  wa  mwisho  waliosimama )  akiwa  katika  picha  ya  pamoja na  baadhi  ya  wanafunzi   na mwalimu wa    Shule  Ya  Sekondari  Ya   Kisaza  iliyopo  Wilayani  Handeni  Mkoani  Tanga. Wanafunzi  wa  Shule  ya  Sekondari  Pangambili  iliyopo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga  wakilima. Wanafunzi  wa  Shule  ya  Sekondari  Pangambili  iliyopo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga.  Wanafunzi  wa  Shule  ya  Kwaludege  Sekondari  wakichota  maji  bwawani  kwa ajili  ya  matumizi mbalimbali. Wanafunzi  wa  Shule  Ya  Sekondari  Kisaza, iliyipo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga. Kabuku  Secondary  School, Handeni, Tanga. Wanafunzi  wa  Kabuku  Sekondari  School, iliyipo  wilayani  Handeni  mkoani  Tanga. Shule  ya Sekondari  Kwaludege  iliyopo  wilayani  Korogwe, mkoani  Tanga. Wanafunzi  wa  Shule  ya Sekondari  Kwaludege  wakiwa  katika  picha  ya  pamoja  na  Katibu  Mkuu  wa